WATU wanne wamefikishwa katika Mahakama Hakimu Mkazi Kisutu kwa tuhuma za kutumia jina la Mke wa Rais, John Magufuli, Janneth Magufuli kutapeli watu. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Watu hao ni pamoja na Saada Uledi, Maftaha, Heshima Ali na Shamba Ali ambao walitumia jina hilo kwenye mtandao wa Facebook kama taasisi ya Janneth Magufuli inayotoa mikopo kwa sharti la kutoa hela kama kinga ya mkopo huo.
Leo tarehe 18 Aprili 2019 Mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonde, wakili wa Serikali Batilda Mushi akisaidiana na Costanine Kakula wamewasomea washtakiwa mashtaka manne.
Shitaka la kwanza ni kula njama ya kutenda kosa ambalo linawahusu watuhumiwa wote. Wanadaiwa kuwa tarehe tofauti Januari mwaka 2017 na Machi 2019 watu hao walitenda kosa la kulanjama ya kuchapisha taarifa za uongo.
Shitaka la pili ni kuchapisha mapachapisho ya uongo linawakabili watuhumiwa wote ambapo inadaiwa walitenda siku tofauti kati ya Januari mwaka 2017 na Machi 2019 ndani ya Jiji la Dar es Salaam.
Watuhumiwa walichapisha kuwa Janneth Magufuli ameunda Taasisi ya inayokopesha watu kwa sharti la kuwataka wakopeshwaji watoe hela kama kinga ya mikopo yao ilhali ni uongo.
Shitaka tatu ni kujipatia fedha kwa njia ya ulaghai watuhumiwa wote wanakabiliwa na shitaka hilo. Inadaiwa walitenda kosa hilo kati ya tarehe 2 Machi 2019 na tarehe 8 Machi 2019 ambapo wakiwa kama waendeshaji wa akaunti ya Facebook yenye jina la Janneth Magufuli walijipatia kiasi cha Sh. 4.4 milioni kwa njia za ulaghai.
Shitaka la nne ni utakatishaji Fedha watuhumiwa wanadaiwa kwa nyakati tofauti kati ya tarehe Januari 2017 na Machi 2019 walifanya utakatishaji kiasi cha Sh4.4 Milioni wakijua kuwa nia zao haramu la ulaghai.
Wakili Batilda amedai kuwa upelelezi haujakamilika mpaka tarehe ya kutajwa. Hakimu Kasonde ameahilisha kesi hiyo mpaka Tarehe 2 Mei 2019.
Leave a comment