SHIRIKA la Ugavi wa Umeme nchini (Tanesco) mkoani Kilimanjaro limekata umeme kwenye hoteli inayomilikiwa na Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema Taifa. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).
Taarifa zinaeleza kuwa, hoteli yake yenye jina la Aish imedaiwa kutumia umeme wa wizi na kusababishia Tanesco hasara ya zaidi ya Sh. 10 million.
Mahawa Mkaka, Meneja Tanesco Mkoa wa Kilimanjaro jana tarehe 14 Septemba, 2018 amesema, hoteli hiyo imejiunganishia umeme na kuharibu miundombinu.
Amesema, walipata taarifa ya wizi huo kutoka katika vyanzo vyao na baada ya uchunguzi wamebaini kuwepo kwa uharibifu na wizi huo.
Mpaka sasa wamiliki wa hoteli hiyo hawajazungumza kuhusu tuhuma hizo
Leave a comment