Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Masikini Mwigulu! Bado yupo kitandani
Habari za Siasa

Masikini Mwigulu! Bado yupo kitandani

Spread the love

MWIGULU Nchemba, Mbunge wa Iramba Magharibi bado yupo kitandani katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma akitibiwa baada ya kupata ajali ya gari. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Ajali hiyo ilitokea jana 13 Februari 2019 katika eneo la Migori, Iringa mbunge huyo akirejea Singida kwa ajili ya kuhudhuria kikao cha kamati ya siasa ya mkoa huo.

Akizungumza namna ajali ilivyotokea Mwigulu amesema, chanzo kikubwa ni dereva wake kukwepa punda watatu waliokuwa wakivuka barabara.

“Dereva wangu wakati anakwepa punda hao waliokuwa wakivuka barabara, alishindwa na baada ya hapo nilisikia kishindo kikubwa. Nilishtuma moshi ukiwa umetanda ndani ya gari ambapo tayari lilimuwa limepinduka,” amesema.

Mwigunu anasema, baada ya ajali hiyo, walitokeawasamaria wema waliomchukua na kumpeleka hospitali kupatiwa matibabu ambapo bado anayendelea na matibabu.

“Nashukuru Mungu naendelea na matibabu, baada ya ajali hilo walionileta hapa ni wasamaria wema,” amesema na kuongeza kuwa, mkanda ulimsaidia kwa kuwa ulikuwa umembana vizuri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!