Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mashtaka 14: Masheikh Uamsho waibwaga Serikali
Habari MchanganyikoTangulizi

Mashtaka 14: Masheikh Uamsho waibwaga Serikali

Spread the love

 

MAHAKAMA ya Rufaa nchini Tanzania, imetupilia mbali rufaa ya Serikali dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kufuta mashtaka 14 katika Kesi ya Jinai Na. 121/2021, inayowakabili Masheikh 23 wa Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu Zanzibar. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo Jumatano, tarehe 19 Mei 2021 na Mwanasheria Kiongozi wa Jopo la Mawakili tisa wanaowatetea Masheikh hao, Juma Nasoro, wakati akizungumza na MwanaHALISI Online.

“Tumeshinda rufaa, masheikh wameshinda, uamuzi ulisema kwamba upande wa Jamhuri hawana haki kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa Mahakama Kuu kufuta mashtaka 14, kwa sababu uamuzi ule haukumaliza kesi,” amesema Nasoro.

Nasoro amesema, kwa sasa masheikh hao wanabaki na mashtaka 11 ya makosa ya ugaidi, katika kesi inayowakabili Mahakama Kuu, wanayodaiwa kutenda katika nyakati tofauti Tanzania Bara.

Wakili huyo amesema, mashtaka 14 yaliyofutwa na Mahakama Kuu, ni yale ambayo makosa yake yanadaiwa kutendwa Zanzibar.

Mahakama ya Rufaa Tanzania

“Baada ya uamuzi huo wa Mahakama ya Rufaa tuanarudi Mahakama Kuu kuendelea na mashtaka ya mwanzo 11, ya makosa yote ya ugaidi yanayodaiwa kufanyika Bara, mashtaka 14 yaliyoondolewa ni yale ya makosa ya ugaidi yanayodaiwa kufanyika Zanzibar,” amesema Nasoro.

Uamuzi wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuwafutia mashtaka 14 masheikh hao, ulitolewa na Jaji Mustapha Ismail, tarehe 23 Aprili 2021.

Masheikh hao wa uamsho walioko mahabusu tangu 2012, wanadaiwa kati ya Januari 2013 na Juni 2014, walijihusisha na makosa ya ugaidi, kinyume na kifungu cha 27 (c), cha Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya mwaka 2002.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Puma Energy Tz: Watanzania tudumishe amani kuvutia uwekezaji

Spread the loveKAMPUNI ya Mafuta ya Puma Tanzania imewakutanisha wadau mbalimbali katika...

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

error: Content is protected !!