Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mashine feki za EFD zaitesa TRA
Habari Mchanganyiko

Mashine feki za EFD zaitesa TRA

Spread the love

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) inateswa na wafanyabiashara wasio waaminifu na wanaotumia mashine feki za kielektroniki za kukusanyia mapato (EFD). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Charles Kichere, Kamishna Mkuu wa TRA amesema, kwa sasa changamoto hiyo ni kubwa ambapo wafanyabiashara hao wamekuwa wakitoa stakabadhi zenye kiasi kidogo cha fedha walizolipa ili kupunguza kodi.

Akizungumza baada ya kufungua mkutano wa washauri wa kodi jijini Dar es Salaam, Kamishna Kichere changamoto hizo ni miongoni mwa sababu za serikali kukosa mapato.

Amkizungumza katika mkutano huo uliolenga kujadili changamoto ya ukusanyaji kodi, Kamishna Kichere amesema kuna mtandao wa baadhi ya watu wanaotengeneza mashine feki za EFD hutoa risiti za kughushi na kupelekea seriali kukosa mapato.

Kamishna Kichere amesema wamebaini uharifu huo wakati wafanyabiashara wanapofanya mrejesho wa kodi, ndipo TRA ilipobaini risiti feki. Amesema tofauti ya risiti halali na feki ni tofauti ya ukubwa wa maandishi.

Katika hatua nyingine, Kamishna Kichere amesema wako baadhi ya watumishi wanaoshughulika na masuala ya kodi sio waamini kwa kuleta  marejesho  yasiyo sahihi, ambapo hupeleka katika Halmashauri, benki na TRA vitabu vya mahesabu vilivyo ghushiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!