Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Masharti Covid-19 yalegezwa Uingereza, mikusanyiko yaruhusiwa
Kimataifa

Masharti Covid-19 yalegezwa Uingereza, mikusanyiko yaruhusiwa

Mashabiki wa soka nchini England wakiwa uwanjani katika moja ya mechi za michuano ya Euro
Spread the love

 

SERIKALI ya Uingereza, imelegeza masharti iliyoweka kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19). Inaripoti BBC…(endelea).

Kwa sasa nchi hiyo imeondoa zuio la mikusanyiko ya watu, matukio ya kijamii, pamoja na kuruhusu sherehe za usiku. Huku uvaaji barakoa ukiwa sio lazima.

Uamuzi wa masharti hayo kulegezwa, ulitolewa jana tarehe 19 Julai 2021 na Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson.

Waziri Mkuu huyo wa Uingereza, alisema sasa ni muda sahihi kwa Taifa hilo kurudi katika utaratibu wa maisha bila ya watu kuwekwa karantini.

Boris Jonhson, Waziri Mkuu wa Uingereza

Mbali ya kulegeza masharti hayo, Johnson aliwataka wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.

“Lakini tunatakiwa kufanya kwa uangalifu, tunatakiwa kukumbuka kwamba virusi hivi kwa bahati mbaya viko nje, visa vinaongezeka. Tunaweza kuona maambukizi ya kirusi cha Delta yakiwa katika kiwango kikubwa,”alisema Johnson.

Waziri wa chanjo nchini humo, Nadhim Zahawi, alisema asilimia 90 ya watu wenye matatizo ya kiafya, wamepatiwa chanjo ya Covid-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Marekani yatia mguu maaandamano Kenya, yatoa maagizo kwa Rais Ruto, Odinga

Spread the love  Mabalozi kutoka nchi sita za Magharibi, zikiongozwa na Marekani,...

Kimataifa

Papa Francis alazwa hospitali kutokana na maambukizi ya mapafu

Spread the love  KIONGOZI wa Kanisa katoliki duniani, Papa Francis jana Jumatano...

Kimataifa

Nyumba ya babu yake Makamu wa Rais wa Marekani yatafutwa Zambia

Spread the love  KAMALA Harris, makamu wa rais wa Marekani, amepanga kutembelea...

Kimataifa

Benki ya Uswizi mbioni kuziwekea vikwazo akaunti za siri za Wachina

Spread the love  WAKATI Serikali na Benki ya Uswizi ikichukua hatua kali...

error: Content is protected !!