Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Masharti Covid-19 yalegezwa Uingereza, mikusanyiko yaruhusiwa
Kimataifa

Masharti Covid-19 yalegezwa Uingereza, mikusanyiko yaruhusiwa

Mashabiki wa soka nchini England wakiwa uwanjani katika moja ya mechi za michuano ya Euro
Spread the love

 

SERIKALI ya Uingereza, imelegeza masharti iliyoweka kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19). Inaripoti BBC…(endelea).

Kwa sasa nchi hiyo imeondoa zuio la mikusanyiko ya watu, matukio ya kijamii, pamoja na kuruhusu sherehe za usiku. Huku uvaaji barakoa ukiwa sio lazima.

Uamuzi wa masharti hayo kulegezwa, ulitolewa jana tarehe 19 Julai 2021 na Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson.

Waziri Mkuu huyo wa Uingereza, alisema sasa ni muda sahihi kwa Taifa hilo kurudi katika utaratibu wa maisha bila ya watu kuwekwa karantini.

Boris Jonhson, Waziri Mkuu wa Uingereza

Mbali ya kulegeza masharti hayo, Johnson aliwataka wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya ugonjwa huo.

“Lakini tunatakiwa kufanya kwa uangalifu, tunatakiwa kukumbuka kwamba virusi hivi kwa bahati mbaya viko nje, visa vinaongezeka. Tunaweza kuona maambukizi ya kirusi cha Delta yakiwa katika kiwango kikubwa,”alisema Johnson.

Waziri wa chanjo nchini humo, Nadhim Zahawi, alisema asilimia 90 ya watu wenye matatizo ya kiafya, wamepatiwa chanjo ya Covid-19.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!