Saturday , 25 March 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Mashabiki wakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya wafuasi wa Arsenal na Manchester City kupigana Uganda
Kimataifa

Mashabiki wakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya wafuasi wa Arsenal na Manchester City kupigana Uganda

Spread the love

 

MASHABIKI wawili wa soka nchini Uganda wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji baada ya mwanamume mmoja kuuawa katika mji mkuu, Kampala kufuatia mzozo wa matokeo ya mechi nchini Uingereza. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Mshauri huyo wa vijana alifariki kutokana na majeraha ya kuchomwa kisu baada ya kuingilia kati kuamua zogo la mashabiki baada ya Arsenal kushindwa na Manchester City siku ya Ijumaa.

Allan Kakumba alifariki muda mfupi baada ya kulazwa hospitalini siku iliyofuata, gazeti la Daily Monitor linaripoti.

Polisi walisema katika taarifa kwamba washukiwa wawili walikuwa kizuizini.

“Tutamfikisha mshukiwa mahakamani hivi karibuni,” Luke Oweyesigire, msemaji wa Polisi wa jiji la Kampala, aliambia BBC.

Bw Oweyesigire alisema Bw Kakumba, 25, aliingilia kati wakati kakake Titus Kyendo, shabiki wa Arsenal, aliponaswa katika vita na wafuasi wa Manchester City.

Haya yanajiri chini ya wiki moja baada ya shabiki wa Arsenal kupigwa hadi kufa huko Adjumani katika wilaya ya West Nile.

Richard Ukuyo alipigwa rungu kisogoni baada ya kumkasirisha mfuasi wa Manchester United aliyeghadhabishwa na ushindi wa Arsenal dhidi yao mwezi uliopita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Rais Tshisekedi amteua kiongozi wa wanamgambo kuwa Waziri wa Ulinzi

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Felix Tshisekedi,...

Kimataifa

Raila Odinga: Tutafanya maandamano makubwa mara mbili kwa wiki

Spread the love KIONGOZI wa upinzani nchini Kenya, Raila Amollo Odinga ametangaza...

Kimataifa

Magharibi kuwekeza silaha Indo-Pacific, China yachochea

Spread the love KUVUNJIKA ushirhikiano wa China na Magharibi uliodumu kwa takribani...

Kimataifa

Ruto amlaumu Odinga kujaribu kuanzisha mgogoro kwa mara ya pili

Spread the love  RAIS wa Kenya William Ruto amesema kwamba hatakubali “kutoijali...

error: Content is protected !!