Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Marekani yatoa tahadhari tishio la Tanzania kushambuliwa
Habari MchanganyikoTangulizi

Marekani yatoa tahadhari tishio la Tanzania kushambuliwa

Spread the love

UBALOZI wa Marekani nchini Tanzania, umeleza kuwepo mipango ya matukio ya mashambulizi kwenye hoteli na migahawa jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kutokana na kitisho hicho, ubalozi huo umetoa tahadhari kwa raia wake waishio hapa nchini kwa kuwataka kuwa makini.

Taarifa hiyo iliyotolewa leo tarehe 19 Juni 2019 imeeleza kuwa, maeneo yaliyolengwa ni kwenye hoteli na migahawa ya kitalii iliyopo Masaki.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa, ubalozi huo umepata tetesi za uwepo wa tishio la kiusalama katika maeneo hayo na kwamba, maeneo lengwa ni yale wanayopenda kutembelewa na watalii pamoja na Duka la Kisasa la Slipway Shopping Center.

Aidha, Ubalozi wa Marekani umesema, hauna uhakika wa kipindi ama muda ambao tukio hilo limepangwa kutokea.

Kufuatia tetesi hizo, imewataka raia wake kuwa na tahadhari.

Ubalozi huo umetoa wito kwa raia wake kuwa makini na maeneo waliyopo, pia maeneo ya kitalii na yanayopendwa na raia wa kigeni, pamoja na kufuatilia taarifa za vyombo vya habari.

MwanaHALISI ONLINE ilimtafuta Kamamda wa Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa kwa njia ya simu kwa ajili ya ufafanuzi wa taarifa hiyo, lakini simu yake kuita bila kupokewa kisha kutokuwa hewani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!