Saturday , 25 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Marekani yaomboleza kifo cha Maalim Seif
Habari za SiasaTangulizi

Marekani yaomboleza kifo cha Maalim Seif

Spread the love

 

UBALOZI wa Marekani nchini Tanzania umesema, Makamu wa kwanza wa Rais Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad (77), alikuwa kiongozi anayeweka mbele watu badala ya madaraka. Anaripoti Matrida Peter…(endelea)

Marekani, umemzungumzia mwanasiasa huyo mkongwe, aliyefariki dunia leo Jumatano tarehe 17 Februari 2021, Hospitali ya Taifa Muhimbili, jijini Dar es Salaam, alipokuwa amelazwa kwa matibabu.

Katika kuraza za kijamii za facebook na Twitter za ubalozi huo, umeweka picha ya Balozi wa Marekani nchini Tanzania, Dk. Donald Wright na Maalim Seif, waliyoipiga hivi karibuni.

Picha hiyo, imeambatana na maneno ya Balozi Wright akisema “ninaungana na Watanzania wote – hususan Wazanzibari – kuomboleza msiba mkubwa wa kuondokewa Maalim Seif.”

“Katika maisha yake akiwa mwanasiasa kwa zaidi ya miaka 40, Maalim Seif amekuwa kielelezo cha kiongozi mtumishi anayewaweka watu mbele kabla ya madaraka. Hatutaweza kuziba pengo lake, lakini tunaweza na ni lazima tuuenzi mchango wake adhimu,” ameandika Balozi Wright

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aagiza iundwe kamati ya pamoja ya Mawaziri mradi wa BBT

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewaagiza mawaziri kuunda kamati...

Habari za Siasa

Rais Samia apangua makatibu tawala mikoa, ateua Kamishna DCEA

Spread the loveALIYEKUWA Kamishna wa Mamlaka ya Kudhibiti Dawa za Kulevya, Gerald...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

M/kiti bodi ya wadhamini Chadema afariki dunia

Spread the loveMWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Zitto: Nikifa Ado atavaa viatu vyangu

Spread the love  KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe...

error: Content is protected !!