Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yahaha kuwasaka wadukuzi wa mitandao
Kimataifa

Marekani yahaha kuwasaka wadukuzi wa mitandao

Spread the love

BARAZA la Usalama la Taifa jijini Washington, Marekani limesema linachunguza shambulio kubwa la kimtandao ambalo limekumba mifumo ya kompyuta duniani kote, anaandika Hamis Mguta.

Mamlaka nchini Marekani zimesema zimedhamiria kuwachukulia hatua wahusika wa uhalifu huo wa mtandaoni, uliosababisha makampuni, taasisi mbalimbali pamoja na watu binafsi kupoteza taarifa zao nyeti baada ya shambulizi la kimtandao.

Mashirika mbalimbali zikiwemo taasisi za kifedha, idara za serikali, makampuni makubwa, na kampuni za usafirishaji ni miongoni mwa zilizoathirika ambapo wadukuzi wa mitandaoni walizishikilia na kuzipoteza taarifa mbalimbali za mitandao.

Wamiliki wa mitandao husika waliambiwa na wadukuzi kuwa kompyuta zao zimenaswa mpaka walipe kiasi cha Dola mia tatu za Marekani katika akaunti isiyofahamika. Huku Wizara ya Mambo ya Ndani ya Marekani ikiwashauri watu wasilipe fedha hizo.

Hata hivyo wizara hiyo imesema hakuna uhakika kwamba, mafaili yaliyofungwa yatafunguka baada ya malipo hayo kufanyika.

Shambulio hilo la kimtandao lilianza nchini Ukraine na linaendelea sehemu nyengine duniani na baadhi ya mashirika yanayoripoti tatizo hilo ni pamoja na Benki kuu nchini humo na kampuni ya kuunda ndege ya Antonov na mashirika mawili ya posta.

Kampuni ya mafuta nchini Urusi ya Rosneft na ile ya Denmark ya Maersk ni miongoni mwa zilizokumbwa na shambulizi hilo la kimtandao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the love  TUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

error: Content is protected !!