Friday , 29 September 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani yahaha kuwasaka wadukuzi wa mitandao
Kimataifa

Marekani yahaha kuwasaka wadukuzi wa mitandao

Spread the love

BARAZA la Usalama la Taifa jijini Washington, Marekani limesema linachunguza shambulio kubwa la kimtandao ambalo limekumba mifumo ya kompyuta duniani kote, anaandika Hamis Mguta.

Mamlaka nchini Marekani zimesema zimedhamiria kuwachukulia hatua wahusika wa uhalifu huo wa mtandaoni, uliosababisha makampuni, taasisi mbalimbali pamoja na watu binafsi kupoteza taarifa zao nyeti baada ya shambulizi la kimtandao.

Mashirika mbalimbali zikiwemo taasisi za kifedha, idara za serikali, makampuni makubwa, na kampuni za usafirishaji ni miongoni mwa zilizoathirika ambapo wadukuzi wa mitandaoni walizishikilia na kuzipoteza taarifa mbalimbali za mitandao.

Wamiliki wa mitandao husika waliambiwa na wadukuzi kuwa kompyuta zao zimenaswa mpaka walipe kiasi cha Dola mia tatu za Marekani katika akaunti isiyofahamika. Huku Wizara ya Mambo ya Ndani ya Marekani ikiwashauri watu wasilipe fedha hizo.

Hata hivyo wizara hiyo imesema hakuna uhakika kwamba, mafaili yaliyofungwa yatafunguka baada ya malipo hayo kufanyika.

Shambulio hilo la kimtandao lilianza nchini Ukraine na linaendelea sehemu nyengine duniani na baadhi ya mashirika yanayoripoti tatizo hilo ni pamoja na Benki kuu nchini humo na kampuni ya kuunda ndege ya Antonov na mashirika mawili ya posta.

Kampuni ya mafuta nchini Urusi ya Rosneft na ile ya Denmark ya Maersk ni miongoni mwa zilizokumbwa na shambulizi hilo la kimtandao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Mahakama yamkuta na hatia Donald Trump

Spread the love  ALIYEKUWA Rais wa Marekani, Donald Trump, amekutwa na hatia...

Kimataifa

Harusi yageuka msiba 100 wakifariki kwa ajali ya moto

Spread the love  WATU takribani 100, akiwemo bibi na bwana harusi, wamefariki...

Kimataifa

Kampuni ya mali ya China Oceanwide yapata agizo la kufilisiwa huko Bermuda

Spread the love  MAHAKAMA ya Bermuda imetoa amri ya kufilisiwa kwa Kamapuni...

Kimataifa

Uvamizi wa kijeshi Milango ya bahari ya Taiwan G7 yapinga China

Spread the loveMKUTANO wa Mawaziri wa Mambo ya nje wa nchi za...

error: Content is protected !!