Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Marekani, China washusha uchumi wa Dunia
KimataifaTangulizi

Marekani, China washusha uchumi wa Dunia

Dola za Marekani
Spread the love

MIVUTANO ya kibiashara ya kidunia imetajwa kuwa miongoni mwa sababu za kushuka kwa uchumi  wa dunia katika kipindi cha mwaka 2018/2019 huku vita ya kibiashara baina ya nchi ya Marekani na China ikihatarisha kuvurugika kwa mwenendo wa biashara za kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kufuatia utafiti wake wa hivi karibuni  inaeleza kuwa, hatua ya Marekani kutangaza viwango vipya vya ushuru pamoja na madeni makubwa, pia imeshusha uchumi wa dunia.

Mchumi Mkuu wa IMF, Maury Obstefeld akizungumzia kuhusu hali ya uchumi duniani, amesema ukuaji wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2018/2019 utasalia katika kiwango cha asilimia 3.7 ambacho ni kiwango pungufu ukilinganisha na asilimia 3.9 kiwango kilichotangazwa mwezi Aprili mwaka huu.

Ripoti ya IMF vile vile imebainisha  kwamba, kiwango cha kukua kwa uchumi wa mataifa yenye uchumi mkubwa duniani, China na Marekani pia kimeshuka.

Ambapo China inatabiriwa uchumi wake kushuka kwa asilimia moja kutoka asilimia 6.4 ilivyo sasa hadi asilimia 6.2 ifikapo mwaka 2019.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!