MIVUTANO ya kibiashara ya kidunia imetajwa kuwa miongoni mwa sababu za kushuka kwa uchumi wa dunia katika kipindi cha mwaka 2018/2019 huku vita ya kibiashara baina ya nchi ya Marekani na China ikihatarisha kuvurugika kwa mwenendo wa biashara za kimataifa. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)
Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa leo na Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) kufuatia utafiti wake wa hivi karibuni inaeleza kuwa, hatua ya Marekani kutangaza viwango vipya vya ushuru pamoja na madeni makubwa, pia imeshusha uchumi wa dunia.
Mchumi Mkuu wa IMF, Maury Obstefeld akizungumzia kuhusu hali ya uchumi duniani, amesema ukuaji wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2018/2019 utasalia katika kiwango cha asilimia 3.7 ambacho ni kiwango pungufu ukilinganisha na asilimia 3.9 kiwango kilichotangazwa mwezi Aprili mwaka huu.
Ripoti ya IMF vile vile imebainisha kwamba, kiwango cha kukua kwa uchumi wa mataifa yenye uchumi mkubwa duniani, China na Marekani pia kimeshuka.
Ambapo China inatabiriwa uchumi wake kushuka kwa asilimia moja kutoka asilimia 6.4 ilivyo sasa hadi asilimia 6.2 ifikapo mwaka 2019.
Leave a comment