MWANAMKE anayedai kuwa ni mchumba, aliyezaa na kuishi na mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM), Timotheo Mnzava, anamtuhumu Mchungaji wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Usharika wa Meru, mkoani Arusha, “kushiriki usaliti wa mchumba wake.” Anaripoti Hamisi Mguta, Dar es Salaam … (endelea).
Mchungaji huyo anayejulikana kwa majina ya Franael Joshua Issangya, anatuhumiwa kuchangia kwa kiwango kikubwa, Mzava kutelekeza familia yake na kutafuta mwanamke mwingine wa kufunga naye ndoa.
Mnzava yuko mbioni kufunga ndoa na Caroline Pallangyo, ambaye ni mtoto wa mbunge wa Arumeru Mashariki (CCM), John Pallangyo.
Ndoa kati ya Mzava na mtoto wa mbunge mwenzake, inatarajiwa kufungwa katika KKKT, Dayosisi ya Kaskazini Mashariki, Usharika wa Mombo, mkoani Tanga, tarehe 10 Julai 2021.
Undani wa nini kimeibuka upya, majibu ya mchungaji huyo anayetuhumiwa na mengine yanayoendelea, soma Gazeti la Raia Mwema, toleo la leo Jumamosi, tarehe 3 Julai 2021.
Leave a comment