Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Mapokezi ya Simba yasimamisha Kigoma
Michezo

Mapokezi ya Simba yasimamisha Kigoma

Spread the love

KIKOSI cha klabu ya Simba, kimewasili mkoani Kigoma kwa ajili ya mchezo wa Fainali wa kombe la Shirikisho dhidi ya Yanga. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo utapigwa siku ya Jumapili, tarehe 25 julai 2021, kwenye Uwanja wa Lake Tanganyika, mkoani humo.

Kikosi cha Simba kiliwasili Kigoma, majira ya saa 12:13 jioni kwa shirika la ndege la Air Tanzania na kupokelewa na mashabiki wao waliojitokeza Uwanjani hapo.

Simba ilianza safari ya kuondoka Uwanjani hapo majira ya saa 12:25 wakiwa na msululu wa mashabiki na kuelekea katikati ya mji.

Kikosi hiko kilitumia Saa 1 kufika kwenye hotel ya Tanganyika ambapo kambi ya timu hiyo ilipo.

Msafara wa Simba uliongozwa na mtendaji Mkuu wa klabu hiyo Barbara Gonzalez, na baadhi ya viongozi wengine waandamizi wa timu hiyo.

Mara baada ya kuwasili Kigoma, kikosi hiko kesho asubuhi kitafanya mazoezi kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Chuo cha Hali ya Hewa.

Yanga ilikuwa ya kwanza kutumia Uwanja juo siku ya jana, katika mazoezi yao ya jionii, na leo klabu ya Simba itafanya pia mazoezi kwenye Uwanja huo huo.

Mara ya mwisho timu hizo zilikutana Julai 3 Mwaka huu kwenye mchezo wa Ligi Kuu soka Tanzania Bara, na Simba kupoteza mchezo huo kwa bao 1-0.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!