Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mapato ATCL yaongezeka
Habari Mchanganyiko

Mapato ATCL yaongezeka

ATCL Dreamliner
Spread the love

MAPATO ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), yameongezeka kutoka Sh. 11.7 Bilioni mwaka 2015/16 hadi Sh. 45.5mwaka 2018/19. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Hayo yamesemwa Dk. Phillip Mpango leo tarehe 13 Juni 2019, wakati akielezea mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Tano katika kipindi cha miaka mitatu, kuanzia mwaka 2016/17 mpaka 2018/19.

Dk. Mpango amesema, mafanikio hayo yametokana na hatua ya Rais John Magufuli kuboresha utendaji wa ATCL, ikiwemo kuongeza idadi ya ndege.

“Uboreshaji huo imesaidia kuongezeka mapato ya ATCL kutoka Sh.11.756 Bil. hadi 45.5632 Bil. Hivi karibuni ATCL,” amesema Dk. Mpango.

Vile vile, Dk. Mpango amesema idadi ya abiria imeongezeka kutoka 49,854 mwaka 2015/16 hadi 242,668 mwaka 2018/19. Pia, miruko (flights) imeongezeka kutoka 672 hadi 3808 mwaka 2018/19, pamoja na idadi ya vituo kutoka kimoja hadi vitano.

Mafanikio mengine aliyotaja Dk. Mpango ni ujenzi wa reli ya kisasa ya Standard Gauge, uboreshaji na ufufuaji wa njia ya reli, ununuzi wa vichwa vya treni 11 vitakavyotumika katika njia kuu na mabehewa 15.

Vile vile, Dk. Mpango amesema mafanikio mengine ni uboreshaji wa huduma za afya kufuatia ujenzi wa hospitali, zahanati, vituo vya afya, na upatikanaji wa dawa za kutosha katika hospitali za umma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

error: Content is protected !!