Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mapambano ya corona: Bunge kumpongeza Rais Magufuli
Habari za Siasa

Mapambano ya corona: Bunge kumpongeza Rais Magufuli

Rais John Magufuli
Spread the love

BUNGE la Tanzania, linatarajia kupitisha azimio la kumpongeza Rais wa nchi hiyo, John Pombe Magufuli, kwa namna alivyoliongoza Taifa katika Mapambano dhidi ya janga la ugonjwa wa Corona (COVID-19). Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Kwa mujibu wa orodha za shughuli za Bunge leo Jumanne tarehe 9 Juni 2020 zilizotolewa na Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai inaonyesha azimio hilo litawasilishwa bungeni leo.

“Azimio la Bunge la kumpongeza Rais John Pombe Magufuli, kwa namna alivyoliongoza Taifa katika Mapambano dhidi  ya Janga la Ugonjwa wa Corona (COVID-19),” inasomeka kwenye orodha za shughuli za Bunge

Kwa mujibu wa taarifa za Serikali ya Tanzania kuhusu hali ya maambukizo ya corona nchini Tanzania zinadai yamepungua.

Bunge la Tanzania

Mgonjwa wa kwanza wa corona alitangazwa tarehe 16 Machi 2020 na mpaka jana Jumatatu, Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu akiwa mkoani Tanga alisema, wagonjwa wamepungua na hivi karibuni watatangaza kutokuwepo kwa mgonjwa yoyote wa corona.

Tayari vyuo vilivyokuwa vimefungwa tangu tarehe 18 Machi 2020 vimefunguliwa kuanzia tarehe 1 Juni 2020 pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita.

Wanafunzi wa kidato cha sita wanajiandaa na mitihani yao ya taifa kuanzia tarehe 29 Juni hadi 16 Julai 2020 na matokeo yanatakiwa kutoka kabla ya tarehe 31 Agosti 2020.

Hivi karibuni, Rais Magufuli alisema kwa hali inavyoendelea, anafikiria kufungua shule za msingi na sekondari ili masomo yaweze kuendelea kama kawaida.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!