TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), inawafikisha watumishi wanne wa Baraza la Taifa la Uhifadhi wa Mazingira (NEMC) katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kwa tuhuma za rushwa na uhujumu uchumi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea)
Watuhumiwa hao ni; Deusdedith Katwale, Magori Matiku na Obadia Machupa ambao wote ni maafisa mazingira na Lydia Nyinondi ambaye ni Mhasibu Msaidizi. Wote wa makao makuu.
Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi tarehe 4 Juni 2020 na Afisa Uhusiano wa Takukuru, Doreen Kapwani imesema, “watuhumiwa hawa, watasomeshwa mashtaka yao katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam,” amesema Doreen
Jana Jumatano, Doreen alitoa taarifa kuzungumzia watuhumiwa hao akitaja tuhuma zinazowakabili ni; kula njama na kutenda kosa, kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo, kuisababishia mamlaka hasara, matumizi mabaya ya madaraka pamoja na utakatishaji wa fedha haramu.
Endelea kufuatilia MwanaHALISI ONLINE kwa habari zaidi
Leave a comment