Tuesday , 5 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Maofisa ugani wapewa somo kuongeza ufanisi
Habari Mchanganyiko

Maofisa ugani wapewa somo kuongeza ufanisi

Mahindi yakiwa shambani
Spread the love

WAZIRI Kilimo, Japhet Hasunga amewataka Maofisa ugani nchini kuweka mipango kazi yao itakayowawezesha kufanikisha ufanisi wa kilimo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Hasunga ametoa kauli hiyo leo wakati akifungua mkutano mkuu wa Mwaka  wa siku moja wa maofisa ugani wa halmashauri zote nchini uliofanyika jijini Dodoma.

Mkutano huo ambao lengo lake kubwa ni kujadili changamoto na kuweka mikakati ya kilimo na mifugo ili kuongeza tija katika sekta hiyo.

Waziri Hasunga alisema kuwa nchi inategemea zaidi maofisa ugani katika kuwezeza mapinduzi ya kilimo na mifugo kwa lengo la kuongeza pato la taifa.

Katika kutekeleza majukumu yao amewataka maofisa ugani kuhakikisha wanawatembelea wakulima na wafugaji kwa lengo la kuwapatia ushauri utakaowawezesha kulima na kufuga kwa njia ya kisasa.

“Inafika hatua unamkuta afisa ugani anamuuliza mkulima kuwa hii ni mbegu gani, yaani baada ya ofisa ugani kumwelekeza mkulima, mkulima anamwelekeza Afisa ugani.

“Tunataka nyinyi maofisa ugani kuwa na takwimu za mashamba ambayo wanayakagua na kutoa maelekezo kwa wakulima kulima kwa kutumia mbegu bora.

“Kama maofisa ugani mtakuwa karibu na wakulima na kuwasaidia vyema ni wazi kuwa kilimo kitaongeza tija na kuwafanya wakulima kulima kilimo cha kisasa zaidi,” alisema Hasunga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

RPC Songwe awafunda trafki kuzingatia uadilifu

Spread the loveASKARI wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Songwe wametakiwa kuendelea...

Habari Mchanganyiko

Mchimba madini jela maisha kwa kubaka, alihonga Sh 500

Spread the loveMahakama ya wilaya ya Songwe imemtia hatiani na kumhukumu kifungo...

Habari Mchanganyiko

Mlima wa Moto wazindua kongamano la SHILO kumuenzi Rwakatare

Spread the loveKANISA la Mlima wa Moto Mikocheni jijini Dar es Salaam,...

Habari MchanganyikoTangulizi

20 wafariki dunia kwa mafuriko Manyara

Spread the loveMVUA za vuli zinazoendelea kunyesha maeneo mbalimbali nchini zimeleta madhara...

error: Content is protected !!