Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mangula amkabidhi Kinana mafaili wanaoanza harakati Uchaguzi 2025
Habari za Siasa

Mangula amkabidhi Kinana mafaili wanaoanza harakati Uchaguzi 2025

Philip Mangula, Makamu Mwenyekiti wa CCM (Bara)
Spread the love

 

ALIYEKUWA Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mzee Phillip Mangula, amemtaka mrithi wake, Abdulrahman Kinana, kuwashughulikia WanaCCM wanaokiuka maadili kwa kuanza mapema mikakati ya Uchaguzi Mkuu wa 2025. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Mzee Mangula amempa maelekezo hayo Kinana, leo Ijumaa, tarehe 1 Aprili 2022, jijini Dodoma, muda mfupi baada ya Mkutano Mkuu Maalumu wa CCM, kumpitisha kwa asilimia 100 kuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho Tanzania Bara.

“Ile kamati ndogo ya udhibiti nakukabidhi Kinana, utakuwa ndiyo mzee wa mafaili. Kwa nini mzee wa mafaili, hivi sasa tumeanza kuangalia wanaochungulia 2025. Ukiona tu kuna dalili fulani unafungua faili, unaanza kuweka kumbukumbu, huyu kasema hiki,”

“Kila mmoja anayeonekana kukiuka taratibu unamfungulia faili ili kuweka kumbukumbu za kinyume na maadili, hayo nimekukabidhi bila shaka unayafahamu pia.”

Akizungumzia kung’atuka kwake katika wadhifa huo, Mzee Mangula amesema hatua hiyo haimaanishi kwamba atajitenga na shughuli za CCM, kwani ataendelea kutekeleza majukumu yake akiwa mjumbe wa Baraza la Ushauri la Viongozi Wakuu Wastaafu.

“Lakini kung’atuka kwangu haimaanishi kutoka kwenye shughuli na uongozi wa chama, kwa nini nasema sitoki? Kwasababu kuna Baraza la Ushauri linaloundwa na viongozi wakuu wastaafu na mimi kuanzia sas ani mjumbe,” amesema Mzee Mangula.

Mzee Mangula amesema aliamua kung’atuka nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, kwa kuwa umri wake ulikuwa unafaa kuwa katika baraza hilo la wastaafu.

“Ibara ya 122 inasema kutakuwa na Baraza la Ushauri la Viongozi Wakuu Wastaafu, wajumbe wote watakuwa wazee kuanzia miaka 60 wanaokubali imani, malengo na madhumuni ya CCM, nikija huko nakuja kama mzee wa miaka hiyo, inaanzia 60 niko 80 nastahili kuwa kwenye baraza,” amesema Mzee Mangula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!