JANETH Magufuli, mjane wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano, Hayati John Magufuli, amesema Rais Samia Suluhu Hassan, amemheshimu kwa kukubali wito wake wa kushiriki hafla ya kumbukizi ya mwaka mmoja wa kifo cha mume wake. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Janeth ametoa kauli hiyo akitoa shukrani za Familia ya Hayati Magufuli, katika hafla hiyo iliyofanyika leo Alhamisi, tarehe 17 Machi 2022, wilayani Chato, Geita, na kuhuduriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na wa dini.
Mjane huyo wa Magufuli, amesema Rais Samia alikubali kushiriki kumbukizi hiyo, licha ya kuwa na majukumu mengi ya kitaifa na kimataifa.
“Naomba nikiri kukupigia simu lakini kwa bahati mbaya sikufanikiwa, ila baadae ulivyonipigia nikakupa mualiko ambao uliupokea kwa moyo mkunjufu na ukaahidi kuja ingawa haikuwa kimaandishi,” amesema Janeth.
Janeth amesema “nashukuru kwa kuja licha ya kuwa una majukumu mengi umeniheshimu sana mama. Tunakuombea kwa Mungu akutie nguvu kuendelea kuliongoza Taifa vyema. Azidi kukujalia afya bora na maisha yako yazidi kuwa mema.”
Aidha, Janeth amewashukuru watu wote walioungana na familia yake, tangu alipofariki dunia tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam, hadi leo inapoadhimisha kumbukumbu ya mwaka mmoja wa kifo chake.
Leave a comment