Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Michezo Manchester United, Villarreal kuminyana fainali Euroa leo
Michezo

Manchester United, Villarreal kuminyana fainali Euroa leo

Spread the love

 

Manchester United leo itashuka dimbani kumenyana na Villarreal kwenye fainali ya kombe la Europa ambao itapigwa kwenye dimba la Gudansk nchini Poland nchini Poland majira ya saa 4 usiku. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Villarreal ambao wanashika nafasi ya saba kwenye msimao wa La Liga wanaingia kwenye fainali hiyo mara baada ya kuwaondosha Arsenal kwenye hatua ya nusu fainali, huku Manchester United ikitinga fainali mara baada ya kuitoa klabu ya As Roma kwa jumla ya mabao 8-5, katika michezo yote miwili.

Kwenye fainali ya michuano hiyo timu za kutoka nchini England zimekuwa hazipati matokeo mazuri kutoka kwa timu zinazotoka nchini Hispania ambapo mara ya mwisho timu iliyopata matokeo kwenye fainali nchini England ilikuwa Liverpool kwenye masimu wa 2000/01 ambapo waliwafunga Alves.

Kuanzia hapo timu hizo kutoka Ligu Kuu nchini England zilipata wakati mgumu mbele ya timu kutoka La Liga ambapo Sevilla alimfunga Middlesbrough, Atletico Madrid ilibuka na ushindi dhidi ya Fulham na hivi karibuni mwaka 2016 Sevilla iliifunga Liverpool.

Manchester United inaingia kwenye mchezo huo wa fainali huku ikiwa na kumbukumbu ya kutwaa taji hilo kwenye fainali yake ya mwisho waliocheza tarehe 24 Mei, 2017 dhidi ya Ajax na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Tusua mkwanja na mechi za Ijumaa leo

Spread the love  LEO hii mechi zinaendelea kote na wewe kama unataka...

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

error: Content is protected !!