HAJI Sunday Manara, Msemaji wa Mabingwa wa Kihistori wa soka nchini Tanzania, Yanga ya jijini Dar es Salaam amesema, wema aliooneshwa na Zacharia Hans Pope, atauenzi kwa kulinda heshima yake. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).
Manara amesema hayo leo Jumatatu, tarehe 13 Septemba 2021, katika shughuli ya kuuga mwili wa Hans Pope kwenye viwanja vya Karimjee, jijini Dar es Salaam. Alifariki 11 Septemba 2021, Hospitali ya Aga Khani jijini humo.
Kabla ya Manara kuhamia Yanga, alikuwa msemaji wa Simba, hali iliyomwezesha kufanya kazi na Hans Pope aliyekuwa mwenyekiti wa kamati ya usajili ya Simba na mjumbe wa bodi ya wakurugenzi wa timu hiyo.
Zaidi alichokizungumza Manara na kile alichokijibu baada ya kuonekana kutofautiana na Hans Pope hadi kuhamiaYanga. Fuatilia hapa:
Leave a comment