Thursday , 18 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Mamlaka ya Sweden yamrejesha raia wa Rwanda
Kimataifa

Mamlaka ya Sweden yamrejesha raia wa Rwanda

Spread the love

 

MAMLAKA ya Sweden imemrejesha Jean Paul Micomyiza mjini Kigali mwenye umri wa miaka 50,raia wa Rwanda aliyekamatwa nchini Sweden mnamo Novemba mwaka 2020 ,kwa tuhuma za mauaji ya kimbari ambayo aliyatekeleza alipokua mwanafunzi wa chuo kikuu. Anaripoti Rhoda Kanuti kwa msaada wa Mashirika ya Kimataifa … (endelea).

Kwamujibu wa taarifa kutoka nchini Rwanda inasema kuwa ,Paul Micomyiza alipokelewa Rwanda siku ya jumatano Aprili 2022 ,nakuipongeza Sweden kwa mchango wake mkubwa wa kupambana bila kujali.

Micomyiza alikamatwa nchini Sweden Novemba mwaka 2020, kwa hati ya kukamatwa ya Rwanda.

Hata hivyo Micomyiza alipoteza rufaa dhidi ya kurejeshwa kwake Desemba mwaka jana, pia ameishi Sweden kwa zaidi ya muongo mmoja .Anatuhumiwa kwa uhalifu wa mauaji ya kimbari kwa jukumu lake la kuwasaka na kuwatambua Watusi ili kulipiza kisasi, baada ya mauaji yaliyofanwa na watusi hao mwaka 1994,alipokua na umri wa mika 22.

Micomyiza hajazungumza lolote kuhusu mashtaka anayokabiliwa nayo nchini Rwanda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

Habari za SiasaKimataifa

Rais Faye amteua aliyekuwa mfungwa mwenzie kuwa waziri mkuu

Spread the loveRais mpya wa Senegal, Bassirou Diomaye Faye, amemteua Ousmane Sonko...

error: Content is protected !!