Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mamia wamuaga Padri Karugendo
Habari MchanganyikoTangulizi

Mamia wamuaga Padri Karugendo

Spread the love

 

MAMIA ya watu wameuaga mwili wa aliyekuwa mwandishi na mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Tanzania, Padri Privatus Karugendo (65). Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Mwili huo umetolewa heshima za mwisho leo Jumatatu tarehe 28 Juni 2021, kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Roho Mtakatifu Segerea, jijini Dar es Salaam.

Padri Karugendo alifariki dunia usiku wa kuamkia tarehe 24 Juni 2021, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, alikokuwa anapatiwa matibabu baada ya kuugua kwa muda mfupi.

Miongoni mwa watu walioshiriki ibada hiyo ni aliyekuwa Mkurugenzi wa Bohari Kuu ya Dawa (MSD), Laurian Bwanakunu na Jennifer John, mke wa Innocent Nashungwa ambaye ni Waziri wa Habari, Sanaa na Michezo pia waziri wa zamani wa ardhi, Anna Tibaijuka.

Akizungumza katika ibada hiyo, amesema kifo cha Padri Privatus kimeacha pigo, kwa kuwa alikuwa mtu muhimu katika familia yake na Taifa kwa ujumla.

“Kupitia kalamu yake, aliweza kutoa maoni ya watu wengi. Alikuwa mwenye hekima na busara, hakuchukia mtu hata kama ulikuwa unatofautiana naye kimtazamo ama maoni,” amesema Jeniffer.

Akisoma wasifu wa Padri Karugendo, Msemaji wa Familia, Emillianus Karugendo amesema alizaliwa tarehe 14 Januari 1956, Bukoba Vijijini mkoani Kagera.

Emillianus amesema, Padri Karugendo ameacha mjane, Rose Birusya na mtoto mmoja, Yesigwe Karugendo.

Baada ya mwili huo kutolewa heshima za mwisho, ulisafirishwa kuelekea makaburi ya Kinondoni mkoani Dar es Salaam, kwa ajili ya mazishi.

Enzi za uhai wake, alikuwa Padri kwa miaka takribani 20 ikiwemo katika Jimbo Katoliki la Rulenge, Parokia ya Buziku mkoani Kagera, alikokuwa Paroko Msaidizi.

Pia alikuwa mwandishi na mchambuzi wa siasa katika gazeti la Mwananchi na Idhaa ya Kiswahili ya Ujerumani, Deutsche Welle.

Mwaka 2009, Padri Karugendo alivuliwa upadri kwa tuhuma za kukiuka maadili ya Kanisa Katoliki.

Mgogoro wa Padri Karugendo na kanisa hilo ulianza kufuatia msimamo wake wa kuunga mkono matumizi ya Kondomu, kwa ajili ya kujikinga maambukizi ya Virusi vya Upungufu wa Kinga Mwilini (Ukimwi).

Miaka minane baadaye tarehe 26 Aprili 2017, alifunga ndoa na mchumba wake Rose Birusya, jijini Dar es Salaam.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

error: Content is protected !!