Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mambosasa: Tumejiandaa kuwashughulikia ipasavyo Ukonga
Habari za Siasa

Mambosasa: Tumejiandaa kuwashughulikia ipasavyo Ukonga

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa
Spread the love

JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limesema litawashughulikia kisheria wale wote wenye lengo la kufanya vurugu siku ya uchaguzi mdogo wa Ubunge utakaofanyika tarehe 16 Septemba 2018 katika Jimbo la Ukonga na udiwani katika Kata ya Vingunguti. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema kuwa jeshi hilo limejiandaa vizuri kusimamia ulinzi na usalama wa raia katika siku hiyo na kuwa kila kituo cha kupiga kura kutakuwa na askari wa vikosi mbalimbali wakifanya doria kila sehemu huku wakiongozwa na askari maalum wa kikosi cha kutuliza ghasia.

“Jeshi halitasita kuchukua hatua za haraka za kisheria kwa mtu yeyote au kikundi cha watu wenye nia ya kufanya vitendo vyovyote ambavyo ni kinyume na kanuni au sheria ya uchaguzi,” amesema.

Mambosasa amesema kuwa wananchi waishio katika jimbo la Ukonga wasiwe na hofu yoyote kwakuwa waliopanga kufanya vurugu watashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.

“Polisi wataendelea kusimamia hadi utoaji wa matokeo ili asitokee mtu akataka kufanya ndivyo sivyo, kuna watu wamekuwa na tabia wakipiga kura wanang’ang’ania sehemu hizo za kupigia kura kwa lengo la kuja kufany vurugu, kwa namna ambavyo tumejipanga atakayejaribu kufanya atakalo ataishia kwenye vituo vya Polisi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Alichokisema Rais Samia baada ya kupokea ripoti ya CAG, TAKUKURU

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Serikali yake itafanyia kazi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

Habari za SiasaTangulizi

Deni la Serikali laongezeka kwa trilioni 11

Spread the loveDENI la Serikali imeongezeka kwa takribani Sh. 11 trilioni sawa...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

error: Content is protected !!