Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Tangulizi Mama wa Kabendera afariki dunia
Tangulizi

Mama wa Kabendera afariki dunia

Spread the love

VERDIANA Mjwahuzi, Mama wa Erick Kabendera, Mwanahabari aliyeko mahabusu akituhumiwa kwa kosa la uhujumu uchumi na utakatishaji fedha, amefariki dunia. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Taarifa ya kifo hicho imetolewa na Familia ya Kabendera,  leo tarehe 31 Desemba 2019.

Kwa mujibu wa familia ya Kabendera, Mama Verdiana amefariki dunia Jumanne ya leo tarehe 31 Desemba 2019, katika Hospitali ya Amana, jijini Dar es Salaam, alikokuwa anapatiwa matibabu.

Wiki mbili kabla ya kifo chake, Mama Verdiana alimuomba Rais John Magufuli kumsamehe mwanaye Kabendera na kumuacha huru, kwa kuwa ndiye msaada na nguzo kwa familia yake.

Mnamo tarehe 13 Desemba 2019 akiwa jijini Dar es Salaam, Marehemu Verdiana aliwaeleza wanahabari kuwa, Kabendera alikuwa anamsaidia kumpa fedha za matibabu, lakini tangu mwanaye huyo alipokamatwa, amekuwa akikosa huduma hiyo muhimu, ikiwemo kutopata dawa kwa wakati.

Kabendera yuko katika Mahabusu ya Gereza la Segerea, tangu alipokamatwa mwezi Julai mwaka huu, akituhumiwa kwa makosa ya Utakatishaji fedha, kukwepa kodi pamoja na kuongoza kikundi cha uhalifu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!