WAWEKEZAJI na wafanyabiashara nchini wameshauri wa kuibua fursa zinazofungamana na sekta ya madini ili ajili kukuza uchumi wa Taifa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).
Wito huo umetolewa leo Jumatatu tarehe 22 Februari 2021 na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassani wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa uwekezaji katika sekta ya madini Tanzania, uliofanyika kwenye Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam.
Mama Samia amewaomba washiriki wa mkutano huo, kujadili namna ya kuifanya sekta hiyo izidi kukuza uchumi wa nchi.
“Natarajia kongamano hili litaibua fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya madini zenye mafungamano na sekta nyingine, mkajaidli jinsi ya kuibua mambo yatakayofanywa na sekta ya madini lakini yatafungamana na sekta ya biashara na nyingine zinazoendana na sekta ya madini,” amesema Mama Samia.
Amewataka washiriki wa mkutano huo, kueleza changamoto wanazokutana nazo katika sekta ya madini ili zifanyiwe kazi na serikali. Huku akiwahimiza kufuata sheria za nchi katika utekelezaji wa shughuli zao.
Hata hivyo, Mama Samia amesema sekta ya madini imeendelea kutoa mchango mkubwa katika mapato ya nchi, na kwamba fedha zilizokusanywa kutokana na shughuli za madini zimekuwa zikiongezeka katika miaka mitano mfululizo, kuanzia mwaka wa fedha wa 2015/2016 hadi 2019/2020.
“Mwaka huu wa fedha 2020/21, wizara ya madini imepangiwa kukusanywa Sh. 526.7 Bil. ambayo ni sawa na wastani wa Sh. 43.89 Bil. kwa mwezi. Takwimu zinaonesha kuwa kipindi cha Julai 2020 hadi Januari 20 21, wizara imekusanya Sh. 360.74 Bil. sawa na asilimia 117 ya lengo la kipindi hiki,” amesema Mama Samia.
“Pamoja na ufanisi huo, mwenendo wa ukusanyaji maduhuli katika kipindi cha miaka mitano imekwenda kwa kukuwa, maduhuli yameongezeka kukusanywa kutoka 2015/2016 hadi 2019/sh. 270 bilioni zilikusanywa 2015/2016 sh 528 bilioni zilikusanywa 2019/2020. Mnaweza kuona ukuaji wa sekta ya madini,” amesema Mama Samia.
Amesema serikali imepanga hadi kufikia 2025, sekta ya madini ichangie asilimie 10 ya pato la taifa.
Leave a comment