Wednesday , 24 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mama Janeth Magufuli amtoa machozi Rais Samia
Habari MchanganyikoTangulizi

Mama Janeth Magufuli amtoa machozi Rais Samia

Spread the love

 

SIMANZI iliyotanda usoni mwa Janeth, Mjane wa Aliyekuwa Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli (61), amemfanya Rais Samia Suluhu Hassan, kutokwa chozi. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Pia, Rais Samia amekuwa akimfariji Mama Janeth ambaye anaonekana mwenye majonzi na kushindwa kukaa vizuri kwenye kiti chake.

Mama Janeth, ameshindwa kujizuia, pindi alipoona msafara uliobeba mwili wa mme wake, Magufuli ukiingia katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma leo Jumatatu, tarehe 22 Machi 2021.

Msafara huo, umeingia uwanjani hapo saa 4:43 asubuhi, ukitoka viwanja vya Bunge, Dodoma ambapo wabunge walipata fursa ya kuuaga mwili wa Dk. Magufuli, aliyefariki 17 Machi 2021, Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam.

Msafara mzima, ulizunguka uwanja mzima mara moja huku umati wote wa waombolezaji wakisimama akiwemo Mama Janeth, aliyekaa kushoto mwa Rais Samia.

Mara baada ya msafara huo kusimama eneo ambalo jeneza lenye mwili wa Dk. Magufuli kushushwa, Mama Janeth alionekana kushindwa kujizuia na kulazima kukaa huku Rais Samia, akionekana kushika kitambaa chake na kujifuta.

Baada ya mwili wa Dk. Magufuli kushushwa na kupelekwa eneop maalum ulipoandaliwa na watu wote kukaa huku Mama Janeth akionekana mwenye majonzi akisaidiwa na wasaidizi wake, Rais Samia, alimfariki kwa kumshika mkono wa kulia.

Hata baada ya kushushwa na kupigwa nyimbo wa Taifa na wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, watu wote walisimama huku Mama Janeth, pekee alikuwa amekaa kwenye kiti chake.

Mara kadhaa, Rais Samia amekuwa akimwona Mama Janeth, amekuwa akitoa kitambaa kujifuta machoni mwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

THRDC yaongeza mkataba wa ushirikiano na ABA

Spread the love  MTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC),...

Habari Mchanganyiko

Rufaa ya Equity Benki, State Oil yakwama

Spread the loveMAHAKAMA ya Rufani, jijini Dar es Salaam, imeshindwa kuendelea na...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari Mchanganyiko

Bodaboda waeleza mafanikio mafunzo usalama barabarani

Spread the loveMADEREVA bodaboda katika Jiji la Dodoma wameeleza jinsi mafunzo ya...

error: Content is protected !!