Friday , 9 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mama aliyejifungua watoto wanne apiga yowe
Habari Mchanganyiko

Mama aliyejifungua watoto wanne apiga yowe

Spread the love

RADHIA Solomon (24), mzazi aliyejifungua watoto wanne kwa pamoja (mapacha) yupo kwenye wakati mgumu wa kukabili changamoto ya kumudu malezi ya watoto hao. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).

Radhia ameieleza MwanaHALISI ONLINE kuwa, hali hiyo inatokana na ukata wa kifedha kwake na mzazi mwenzake.

Amesema “watoto hawa wanatumia maziwa ya kopo ambapo wanatumia kopo moja kwa wiki. Kopo hilo linagharimu shilingi elfu 40  ambapo  sisi tunashindwa kumudu.”

Ameomba kwa watu wataokaoguswa, wamsaidie taulo za watoto, maziwa na huduma za afya  sambasamba na mazingira anayoyatumia kuwalea watoto hawa.

Amesema, licha kuwa serikali kuweka utaratibu kwa mzizi atakayejifungua watoto zaidi ya wawili atasaidiwa na kwenye malezi lakini yeye ni mwezi wa pili hajapata msaada ingawa alifika Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kinondoni kujieleza.

Kwa yoyote atakayeguswa na hili awasiliane na Radhia kwa namba 0682 604 202.

Tazama video hapo chini kujua alichosema Mama huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!