Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mama aliyejifungua watoto wanne apiga yowe
Habari Mchanganyiko

Mama aliyejifungua watoto wanne apiga yowe

Spread the love

RADHIA Solomon (24), mzazi aliyejifungua watoto wanne kwa pamoja (mapacha) yupo kwenye wakati mgumu wa kukabili changamoto ya kumudu malezi ya watoto hao. Anaripoti Faki Sosi… (endelea).

Radhia ameieleza MwanaHALISI ONLINE kuwa, hali hiyo inatokana na ukata wa kifedha kwake na mzazi mwenzake.

Amesema “watoto hawa wanatumia maziwa ya kopo ambapo wanatumia kopo moja kwa wiki. Kopo hilo linagharimu shilingi elfu 40  ambapo  sisi tunashindwa kumudu.”

Ameomba kwa watu wataokaoguswa, wamsaidie taulo za watoto, maziwa na huduma za afya  sambasamba na mazingira anayoyatumia kuwalea watoto hawa.

Amesema, licha kuwa serikali kuweka utaratibu kwa mzizi atakayejifungua watoto zaidi ya wawili atasaidiwa na kwenye malezi lakini yeye ni mwezi wa pili hajapata msaada ingawa alifika Ustawi wa Jamii Wilaya ya Kinondoni kujieleza.

Kwa yoyote atakayeguswa na hili awasiliane na Radhia kwa namba 0682 604 202.

Tazama video hapo chini kujua alichosema Mama huyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!