Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Malinzi ateuliwa kuwa Mjumbe wa FIFA
Michezo

Malinzi ateuliwa kuwa Mjumbe wa FIFA

Jamal Malinzi, Rais wa TFF
Spread the love

JAMAL Malinzi Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) ameteuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) kuwa mmoja kati ya wajumbe wa Kamati ya Maendeleo ya soka katika kipindi cha miaka minne.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa kwa TFF, iliyosainiwa na katibu mkuu wa FIFA, Fatma Samoura, ilisema uteuzi huo unaanza mwaka huu 2017 mpaka 2021 huku majukumu ya kamati hiyo ni kusimamia mipango ya mpira wa miguu duniani kote.

Kamati hiyo ambayo itaongozwa na Sheikh Salman Bin Ebrahim Al Khalifa ambaye ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Asia itakuwa na wajumbe wengine kutoka nchi wanachama wa FIFA ambao watatangazwa kupitia mtandao wa shirikisho hilo.

Huu utakuwa mfululuzo kwa Malinzi kuteuliwa katika kamati tofauti za mashirikisho ya kimataifa ya mipra wa miguu, mwaka jana shirikisho la soka barani Afrika CAF lilimteua Malinzi kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati maalumu iliyoongozwa na Rais wa shirikisho hilo Issa Hayatou.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!