Thursday , 25 April 2024
Home Habari Mchanganyiko “Mali za ushirika zilizopigwa zawekewa mikakati”
Habari Mchanganyiko

“Mali za ushirika zilizopigwa zawekewa mikakati”

Moja ya mali za Chama cha Ushirika cha Mwanza (Nyanza)
Spread the love

SERIKALI imekiagiza Chama Kikuu Cha Ushirika (Nyanza) mkoani Mwanza kuhakikisha kinaorodhesha na kuzitambua mali zote  za chama hicho zilizokuwa zimetaifishwa kinyemera. Anaripoti Moses Mseti, Mwanza … (endelea). 

Imesema mali zote za Nyanza ambazo tayari zimerejeshwa kwenye chama hicho, pia zinapaswa kukatiwa hati miliki hatua ambayo itasaidia kuzitambua na kuondoa mianya ya upigaji.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa mkoa wa Mwanza, John Mongella, wakati wa mkutano mkuu wa 27 wa chama cha kikuu cha ushirika Nyanza uliofanyika jijini Mwanza.

Mkuu huyo wa mkoa ambaye aliwakilishwa na Mkuu wa Wilaya ya Sengerema, Emmanuel Kipole, alisema mali zote zilizopo zinapaswa kulindwa na kuboreshwa na kutangazwa ili zipate wawekezaji.

“Mali zilizopo zinatakiwa kuboreshwa na zitangazwe kwa ajili ya kupata wawekezaji kwa ajili ya kusaidia uendelezwaji wake kwa manufaa ya chama na umma kwa ujumla.

“Mali ambazo pia hazina bima zikatiwe bima mapema iwezekanavyo na zile hujuma zote ambazo zilikuwa zinafanywa na viongozi ziachwe mara moja,” alisema Kipole.

Meneja mkuu wa Chama Kikuu Cha Ushirika Nyanza, Juma Mokili, alisema kuwa thamani za mali zote za chama hicho zilizorejeshwa ni zaidi ya Sh. 15. 853 bilioni.

Alisema kuwa baada ya Rais John Magufuli kuagiza mali za Nyanza kurejeshwa mwaka 2017, tayari walianza kazi hiyo kwa ushirikiano wa ofisi ya Mkuu wa mkoa pamoja na wizara ya kilimo.

Mokili alisema tayari urejeshwaji wa mali hizo umefanyika kwa asilimia 99 na kwamba Machi mwaka huu mali zote ambazo hawajapewa hati zake watakuwa wamekabidhiwa.

Alizitaja baadhi ya mali ambazo zimerejeshwa kuwa ni pamoja na kiwanda cha New Era, jengo la Kauma kilipo kituo cha mafuta cha City Filling Station na kiwanda cha mkonge na Dengu Igogo Mwanza.

“Mali nyingine zilizorejeshwa ni maghara ya mazao kilichopo katika kiwanja namba 104, nyumba tatu zilizopo Isamilo katika viwanja namba 89, 80 na 110,” alisema Mokili.

Mkutano huo uliokuwa na kauli mbiu “ushirika ni afya na uzingatiaji kanuni 10 za kilimo bora cha pamba utawezesha uzalishaji wenye tija,” umewakuta wadau wa kilimo na viongozi mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!