Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Maleria yaahirisha kesi ya wafugaji, askari
Habari Mchanganyiko

Maleria yaahirisha kesi ya wafugaji, askari

Spread the love

MAHAKAMA ya Mwanzo Mikongezi, Mvomero imelazimika kuahirisha kesi ya kujeruhi iliyowahusisha wafugaji watatu waliowajeruhi askari wanyamapori sehemu mbalimbali za miili yao baada ya mashahidi wanne upande wa washtakiwa kutofika mahakamani wakidaiwa kuumwa ugonjwa wa Malaria. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

Hakimu wa Mahakama hiyo, Mussa Lilingani alisema, amelazimika kuahirisha kesi kutokana na mashahidi hao kutofika mahakamani ambapo aliagiza itolewe hati ya kukamatwa kwa washtakiwa wengine watatu ambao walikimbia baada ya tukio hilo.

Awali Hakimu huyo aliwataja washtakiwa hao kuwa ni Sperwa Kisakiri, Daniel Babalai na Kashuma Kishaki ambapo alisema, siku ya tukio washtakiwa hao waliwajeruhi Emmanuel Willnely na Exavery Pius ambao ni askari wa kamati ya wanyamapori ya maliasili ya kijiji, kwenye msitu wa hifadhi wa asili wa kijiji cha Kihondo kata Doma wilayani humo walipokuwa wakiondoa mifugo iliyoingia hifadhini kinyume cha sheria.

Tukio hilo lilitokea Oktoba 8 mwaka huu katika msitu huo wa hifadhi ambapo Kesi ya kujeruhi namba 115/2019 yenye kifungu namba 228 ilisomwa kwa mara ya kwanza mahakamani hapo Oktoba 11, ambapo itasikilizwa tena Oktoba 30 mwaka huu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!