Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Makontena ya makinikia sasa kuuzwa
Habari Mchanganyiko

Makontena ya makinikia sasa kuuzwa

Spread the love

HATIMAYE Rais John Magufuli ameagiza makontena 277 ya makinikia, yaliyozuiwa katika Bandari ya Dar es Salaam, kwa zaidi ya miaka miwili yauzwe. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Amesema, baada ya kuuzwa fedha zipelekwe kwenye Kampuni ya Madini ya Twiga, inayomilikiwa na serikali pia Kampuni ya Madini ya Barrick.

Rais Magufuli ametoa agizo hilo leo tarehe 24 Januari 2020, jijini Dar es Salaam, katika hafla ya utiaji saini mkataba wa madini baina ya Serikali ya Tanzania na Kampuni ya Madini ya Barrick.

“Yale Makontena ambayo yako bandarini ambayo tuliyashika sasa mkatafute wabia mkayauze, kwa faida ya Kampuni ya Twiga,” ameagiza Rais Magufuli.

Makontena hayo, yalizuiwa bandarini mwaka 2017, yakiwa njiani kusafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya kuchenjuliwa.

Rais Magufuli alizuia yasisafrishwe baada ya kubaini kuwepo udanganyifu wa viwango vya madini vilivyomo katika makinikia hayo. Kisha aliunda Kamati Maalumu ya Uchunguzi wa Mchanga wa Madini uliomo katika makontena hayo.

Kamati hiyo ya wajumbe wanane iliyoongozwa na Profesa Abdulkarim Mruma, ilibaini kwamba katika makinikia hayo kulikuwa na viwango vingi vya madini hasa ya dhahabu, tofauti na viwango vilivyo vilivyoripotiwa serikalini.

Kufuatia sakata hilo, Rais Magufuli alimfuta kazi Sospeter Muhongo, aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini wakati huo, pamoja na kuivunja Bodi ya Wakala wa Ukaguzi wa Madini nchini (TMAA).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!