Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda: Nichagueni, nazifahamu changamoto za Kigamboni
Habari za Siasa

Makonda: Nichagueni, nazifahamu changamoto za Kigamboni

Paul Makonda
Spread the love

ALIYEKUWA Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salam, Paul Makonda amesema ana uwezo wa kuyatekeleza yale yote yaliyomo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na yakatokea. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Makonda ametoa kauli hiyo leo Jumatatu tarehe 20 Julai 2020 katika mkutano mkuu wa CCM Jimbo la Kigamboni, Dar es Salaam unaofanyikia ukumbi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere, Kuvukoni wenye lengo la kupiga kura za maoni jimbo hilo.

Wagombea watakaopigiwa kura ni 78 akiwemo mbunge anayemaliza muda wake, Dk. Faustine Ndugulile.

Akijinadi kwa wajumbe wa mkutano huo, Makonda amesema, “najua changamoto tulizonazo, ninao uzoefu wakutosha na si tu kwa kuongoza bali kwa kutatua changamoto, ninayo picha ya changamoto zote za Jimbo kwakuwa nilikuwa kiongozi ndani ya chama.”

Sylvester Mjuni ‘Mpoki’

“Nimepita na nimeona hali ambayo hairidhishi ya ofisi zetu, nitahakikisha kila kata iwe na mfuko wake au Saccos yake ili kumwezesha kiongozi husika afanye kazi kiwepesi.”

Makonda ni mgombea namba 38 katika kitabu cha wagombea ambapo kwa mujibu wake mwenyewe amewaambia wajumbe kuwa wakisahau jina lake kwenye kumpigia kura basi wakumbuke miaka ambayo ameitaja kuwa ni 38.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online na MwanaHALISI TV kwa habari zaidi

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

Habari za SiasaTangulizi

Maafa Manyara: Rais Samia akatisha ziara yake Dubai

Spread the loveRAIS wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan, amekatisha ziara yake...

Habari za SiasaTangulizi

Wataalaam wa miamba watua Hanang

Spread the loveWaziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na...

error: Content is protected !!