Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Makonda: Mashoga wamekimbia Dar, wamehamia Dodoma
Habari Mchanganyiko

Makonda: Mashoga wamekimbia Dar, wamehamia Dodoma

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda
Spread the love

MKUU wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema kuna baadhi ya watu wanaofanya biashara ya kuuza mwili (machangudoa na mashoga) wamehamia Dodoma ili kutafuta soko. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Makonda ameyasema hayo wakati akizungumza na wanahabari leo tarehe 31Oktoba 2018 jijini Dar es Salaam.

Amesema, tangu serikali itangaze Dodoma kuwa makao makuu ya nchi, kuna watu walishaanza kutangulia mkoani humo, ambapo wengi wao wanatoka jijini Dar es Salaam.

“Na kama mnakumbuka pale waliposema makao makuu ya nchi yanakuwa Dodoma kuna watu walishaanza kutangulia Dodoma kama sehemu ya kujua soko lao linapatikana kule, na hao wanaofanya hivyo wanatoka Dar es Salaam,” amesema na kuongeza.

“Kuna watu wametoka Buguruni wameanzisha madanguro yao Bagamoyo, Mpanda Arusha  na Dodoma.Sio jambo jema.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!