Saturday , 10 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Makonda: Kwa mvua hizi, kuweni na tahadhari
Habari Mchanganyiko

Makonda: Kwa mvua hizi, kuweni na tahadhari

Spread the love

KUFUATIA mvua zinazoendelea kunyesha, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amewataka wakazi wa mkoa wake kuwa na tahadhari  ili kuhepuka mafuriko. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Makonda ametoa kauli hiyo leo tarehe 9 Oktoba 2019, wakati akizindua mfumo wa kupokea kero za wananchi na malalamiko dhidi ya watendaji.

“Tunazidi kuwasihi sana wananchi kujenga kwa kufuata mipango miji, lakini pamoja na jitihada ambazo serikali imeendelea nazo naomba niwasihi wananchi kuona umuhimu wa kufanya usafi,” amesema.

Amesema, kwa mujibu wa Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini (TMA), mvua zitaendelea kunyesha zaidi na kwa sababu mji huo upo chini kutoka usawa wa bahari, wananchi wanapaswa kuwa makini hasa wanaoishi mabondeni.

“Nawapa pole wanaopata changamoto na ni vyema tukaendelea kujihadhali na kuchukua hatua mapema iwezekanavyo,” amesema.

https://youtu.be/PjpsO_T1OK4

Katika hatua nyingine Makonda amezindua mfumo maalum wa kufikisha malalamiko kwa njia ya ujumbe mfupi wa maneno kupitia namba ambazo kila wilaya imepewa.

“Kutuma ujumbe huu ni bure ambapo unatuma ujumbe kwa kuanza na neni DSM na kuandika ujumbe wako kisha unatuma kwenda namba 11000 au kwa wanaotumia mtandao wanaweza kutuma malalamiko yao kupitua www.malalamiko.dsm.go.tz,” amesema.

Kwa upande wa Katibu Tawala Mkoa wa Dar es Salaam, Abubakar Kunenge amesema kuwa kadri ambavyo mfumo huo utaendelea kutunika, unakubali kuongeza mahitaji mengine kadri yatakavyohitajika kulingana na wakati husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Askari Polisi zaidi ya 100 wapigwa msasa wa udereva kukabiliana na ajali

Spread the love  KATIKA kuhakikisha wimbi la ajali za barabarani zinapungua kama...

Habari MchanganyikoTangulizi

Serikali yakana kuhamisha kwa nguvu jamii ya Kimasai Loliondo

Spread the loveWAZIRI wa Katiba na Sheria nchini Tanzania, Dk. Damas Ndumbaro,...

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

error: Content is protected !!