Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda kujitosa ubunge, mjadala waibuka
Habari za Siasa

Makonda kujitosa ubunge, mjadala waibuka

Paul Makonda, Mtia nia jimbo la Kigamboni
Spread the love

HATUA ya Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, kuchukua fomu ya kuomba kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), kugombea ubunge katika Jimbo la Kigamboni, imeibua maswali. Anaandika Faki Sosi, Dar es Salaam…(endelea).

Makonda amechukua fomu hiyo leo tarehe 15 Julai 2020, jijini Dar es Salaam huku hoja kubwa iliyoibuka kwenye mitandao ya kijamii ni kuhusu kama amejiuzulu ama la.

Tayari Rais John Magufuli alitoa onyo kwa wateule wake wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali kwenye ngazi mbalimbali, nafasi zao hazitawasubiri.

Rais Magufuli alisema, mteule wake atakayeomba ruksa kwenda kugombea atampatia na nafasi yake itajazwa pasina kusubiri kurejea baada ya mchakato wa kupata wagombea kukamilika.

Mjadala kwenye mitandao ya kijamii hususani twitter, umejielekeza kuhusu kujiuzulu kwake lakini pia nafasi ya Dk. Faustine Ndungulile, aliyekuwa Naibu Wazir wa Afya, ambaye ndiye mbunge anayemaliza muda wake kwenye jimbo hilo.

Soma zaidi hapa

Uchaguzi Mkuu 2020: JPM ‘Ukiniomba ruhusa nakupa lakini…’

Mtu anayejitambulisha kwa jina la @JengelaChriss, ameandika “kwa hiyo amepumzika ukuu wa mkoa au bado anaendelea na nafasi yake ya ukuu wa mkoa huku akisubiri kuteuliwa kuwa mgombea wa nafasi ya ubunge?”

Jonahbmz kwenye ukurasa wake wa twitter ameandika, “mzee baba si alisema wajiuzulu kwanza? au nilisikia vibaya?” ameuliza.

Timothy96830693 amehoji kwamba, kwanini wakuu wa mikoa nao wanakimbilia ubunge na kwamba, Dodoma kuna nini?

“Sasa mbona kila mtu analimbilia Dodoma, kuna nini? Kwa nia njema au maslahi binafsi? Maana sasa Ukuu wa Mkoa mpaka Ubunge.”

FredOyoo9 amehoji “Duh! Kwa hyo kero za wanaKigamboni atazipelekea mkuu wa mkoa wa Dar?”

@abubadohu ameuliza “Mkuu wa Mkoa ameachia ngazi ya cheo chake au mpaka apitishwe?”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!