Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda: Kama si njaa, ningejiuzulu
Habari za Siasa

Makonda: Kama si njaa, ningejiuzulu

Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema, kama isingekuwa njaa, basi angefanya uamuzi wa kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kukosolewa na Rais John Magufuli. Anaripoti Martin Kamote … (endelea).

Amesema, aliona haya pale Rais Magufuli alipomkosoa kuhusu kusuasua kwa miradi ya ujenzi wa Machinjio ya Vingunguti na Fukwe ya Coco Beach.

Akizungumza katika hafla ya kuwadhamini wanafunzi 100 wa Kidato cha IV mchepuo wa Sayansi, wanaotoka katika familia masikini leo tarehe 17 Septemba 2019 jijini Dar es Salaam, Makonda amesema, njaa ndio iliyomfanya asijiuzulu.

Makonda ameeleza, kauli hiyo iliyotolewa na Rais Magufuli jana tarehe 16 Septemba 2019, ilikuwa ni aibu na kuwa kama asingekuwa na njaa kali, leo angandika barua ya kujiuzulu.

Aidha, Makonda amedai kwamba kuna baadhi ya wanasiasa jijini humo wanakwamisha utekelezwaji wa miradi kadhaa, wakitaka kupatiwa rushwa.

Kufuatia changamoto hiyo, Makonda amesema anaunda kamati maalumu kwa ajili ya kusimamia utekelezaji wa miradi ya kimkakati katika mkoa wa Dar es Salaam. Wajumbe watakaokuwa katika Kamati hiyo ni pamoja na maafisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Tanzania (TAKUKURU).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!