Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Makonda: Bila Neno la Mungu, Magereza, polisi hawatatosha
Habari MchanganyikoTangulizi

Makonda: Bila Neno la Mungu, Magereza, polisi hawatatosha

Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amesema, Magereza na Polisi hawatatosha iwapo Neno la Mungu halitafanya kazi. Anaripoti Regina Mkonde…(endelea).

Amesema kuwa, gharama za kujenga uzio mkubwa, mageti zinaweza kuzuiwa ama kupunguzwa iwapo tu watu wataishi na Neno la Mungu.

Makonda ametoa kauli hiyo leo jioni tarehe 26 Desemba 2018 wakati akizungumza kwenye Mkutano wa Kujenga Umoja wa Viongozi wa Dini uliofanyika kwenye ukumbi wa Mliman City, jijini Dar es Salaam.

“Polisi hawatatosha, magereza hawatatosha endapo tutafanyia kazi ya dini.

“Kama Neno la Mungu litasimama hatutahitaji kuweka mageti, fensi. Gharama hizo zinaweza kuepukwa,” amesema Makonda.

Hata hivyo Makonda ameonesha kutofurahishwa na habari mbaya za viongozi wa dini ambazo huharibu sifa ya kanisa.

Amesema, mengine yanatokea kutokana na watu kutotii viongozi wa dini na kwamba, hofu hiyo imewatoka.

“Hivi Biblia hi ndio ya zamani? Ndio ile ninayoijua? Ifike mahali mtu akiitwa na askofu asijiulize.

“Mchungaji anatembea na house girl (dada wa kazi) tunakaa kimya,”anasema Makonda.

Pia Makonda amewaomba viongozi hao wa dini pamoja na kuwapa watu neno la Mungu, wawaeleze na maisha yao.

“Kama serikali inasema tunaenda vizuri bado na wewe unapaswa kumuonesha,” amesema.

Ameelezea namna Rais John Magufuli alivyoingia na kupindua baadhi ya mambo kwa maslahi ya nchi ikiwa ni pamoja na sekta ya madini.

“Rais Magufuli aliona bora awe mpole pale CCM kabla ya kuingia, maana angeweza kuzuiliwa. Sasa ameingia na amepindua,” amesema.

Ameeeleza kuwa, Rais Magufuli amefanya mengi ambayo watu wasingependa yafanywe kwa kuwa wengi waliishi kwa mazoea.

“Kuna baadhi ya mambo amekuwa akifanya mimi najiulize ningeweza kufanya? Kwa mfanyo haya masuala ya mchanga wa madini na namna mtikisiko wake ulivyokuwa.

“Mnajua kwamba tulikuwa hatuwezi hata kukondroo (kuongoza) ndege zetu wenyewe? Sasa hivi ndio anajenga. Tumwombee,” amesema Makonda.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

error: Content is protected !!