Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Makonda amvimbia mteule wa JPM
Habari za Siasa

Makonda amvimbia mteule wa JPM

Spread the love

PAUL Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, amefutilia mbali kauli ya Sofia Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Ilala kwamba ibada zifanywe siku maalum tu. Anaripoti Martin Kamote…(endelea).

Makonda ametangaza uamuzi huo mbele ya waandishi wa habari leo tarehe 22 Oktoba 2019, ofisini kwake huku akisisitiza ‘umakini kwa viongozi wa serikali kuzungumzia imani za dini.’

Tarehe 12 Oktoba2019, Mjema aliwaagiza maofisa kwenye wilaya yake kuhakikisha, ibada zinafanywa kwenye siku maalum (Ijumaa, Jumamosi na Jumapili) na si vinginevyo.

Akipingana na kauli hiyo, Makonda amesema, vingozi hawapaswi kuingilia siku za wananchi kuabudu na badala yake, wanapaswa kuwa makini wanapotaka kuzungumzia masuala ya imani.

“Viongozi tunapaswa kuwa makini tunapoingia kwenye mambo ya dini, mambo ya dini ni mambo ya imani, mimi mwenyewe hapa ni mlokole hunipangii muda wa kusali,” amesema Makonda na kuongeza “kwa kuwa mimi ndio mkuu wa mkoa huu, ibada nazitaka siku zote.”

Tazama video kamili hapo chini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!