Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Makocha 55 wajitosa kumrithi Sven Simba
Michezo

Makocha 55 wajitosa kumrithi Sven Simba

Sven Vandenbroeck
Spread the love

KLABU ya Simba ya jijini Dar es Salaam nchini Tanzania imesema, makocha 55 wametuma wasifu (CV) wakiwania nafasi moja ya kuwafundisha mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Kwa sasa, Simba inafundishwa na kocha msaizidi, Suleiman Matola, baada ya aliyekuwa kocha wake mkuu, Sven Vandenbroeck kuachana na timu hiyo kwa makubaliano ya pande zote mbili Alhamisi tarehe 7 Januari 2021.

Wakati Sven akisema, ameachana na Simba ili kumwezesha kuwa na uwiano kati yake na kazi, familia na maendeleo binafsi, jana Jumamosi, Klabu ya FAR Rabat inayoshiriki Ligi Kuu nchini Morocco, ilimtangaza Sven kuwa kocha wake mkuu kwa mkataba wa miaka miwili.

Barbara Gonzalez,Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba

Jana Jumamosi tarehe 9 Januari 2021, Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez alisema, wanaendelea na uchambuzi makini ili kumpata kocha bora atakaowafikisha kwenye malengo waliojiwekea na hawatokuwa na haraka kwenye mchakato huo.

Barbara alisema, wameweka masharti ikiwemo uzoefu wa kocha kwenye timu za taifa, mashindao ya Shirikisho la Soka Afrika kwa maana ya Klabu Bingwa na Kombe la Shirikisho.

“Mpaka sasa kuna walimu 55 ambao wameomba kazi. Tunaendelea na uchambuzi ili kumpata kocha sahihi kwa ajili ya timu yetu na tumekwisha kuweka masharti fulani ikiwemo uzoefu wake kwenye kazi kama timu za Taifa na mashindano ya CAF,” amesema Barbara.

Amesema, hawatakuwa na haraka ya katika kufanya uchambuzi lengo ni kumpata kocha bora ili wasije kumpata kocha ambaye anaweza “kuharibu mipango yetu ya Ligi ya Mabingwa na mashindano mengine.”

Ofisa mtendaji mkuu huyo amesema, katika kipindi chote, timu hiyo itaendelea kuwa chini ya kocha msaidizi, Suleiman Matola.

Simba kwa sasa iko visiwani Zanzibar katika michuano ya mapinduzi ikiwa imeshunda uwanjani mara mbili dhidi ya Chupukizi na kuifunga 3-1 na jana ilicheza na Mtibwa Sugar na kuifunga 2-0.

Hadi Sven anaondoka, ameiacha imefuzu hatua ya makundi ya Klabu Bingwa Afrika ikiwa imepangwa kundi A pamoja na timu za Al Merrikh (Sudan), AS Vital (DRC Congo) na Al Ahly ya Misri.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!