Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Makamu wa Rais Gambia ajiuzulu
KimataifaTangulizi

Makamu wa Rais Gambia ajiuzulu

Isatou Njie, Makamu wa Rais wa Gambia
Spread the love

ISATOU Njie, Makamu wa Rais wa Gambia ametangaza wazi kuachia ngazi hiyo kufuatia sintofahamu ya hali ya kisiasa iliyotanda katika Taifa hilo la Afrika Magharibi, anaandika Wolfram Mwalongo.

Hatu hiyo imekuja wakati tayari Mawaziri zaidi ya saba wamejiuzulu, hali hiyo imetokana na uamzi wa Rais Yahya Jammeh kutangaza wazi kwamba hawezi kuachia nchi kwa mpinzani wake Adama Barroa aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi Mkuu wa mwaka jana.

Rais Jammeh amekataa katu kuondoka Ikulu ya nchi hiyo kwakile alichodai kwamba uchaguzi uliompa ushindi mpinzani wake uligubikwa na kasoro hivyo anataka urudiwe.

Bunge la nchi hiyo limetangaza kumwongezea muda kiongozi huyo huku Wafuasi wa Barrow wakishutumu maamzi hayo kwa kile wanachodai bunge la nchi hiyo limeshindwa kusimami misingi ya sheria.

Kwa mjibu wa Shirika la habari la Al Aljazeera Adama Barrow ambaye alipaswa kuingia Ikulu ya Gambia hii leo, anatarajiwa kuapishwa ubalozini nchini Senegal.

Wakati huo vikosi vya kijeshi kutoka mataifa mbalimbali ya  Jumuhiya ya kiuchumi ya Afrika magharibi (ECOWAS) vimeendelea kutia nanga kwenye Ardhi ya Gambia ikiwa ni maandalizi ya kumung’oa kwa mtuu Rais Jammeh.

Ousman Badjie Mkuu wa majeshi wa Gambia hivi sasa ameonekana kujiweka kando na Rais Jammeh kwakile alichodai kuwa hatathubutu kuruhusu majeshi yake kufanya mashambulizi kwa yeyote.

Huku akionekana kubadili msimamo wake wa awali ambapo Jenerali huyo alitangaza wazi kumuunga mkono Rais aliyemadarakani.

Wagambia wameendelea kukimbia nchi yao na kuingia nchini Senegal kwakuhofia machafuko kutokana na azma ya Wafuasi wa Barrow kumtangaza Rais Jammeh kuwa “muasi”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!