MAKAMU wa rais wa Afghanistan, Jenerali, Abdul Dostum amezuiwa kuingia nchini mwake akitokea nchini Uturuki, anaandika Mwaandishi wetu.
Ndege ya kiongozi huyo iliyojaribu kutua nchini humo ikitokea Uturuki imezuiwa.
Dostum alijaribu kurudi nchini humo baada ya kusafiri kuelekea Uturuki mnamo mwezi Mei huku kukiwa na madai kwamba aliwaagiza watu wake kumteka, kumpiga na hata kumbaka mpinzani wake wa kisiasa.
Hata hivyo, amekana kufanya makosa yoyote na kuwa alielekea nchini humo kwa ukaguzi wa afya yake.Haijulikani ni nani aliyekataza kutua kwa ndege hiyo lakini taarifa za karibu na rais Ashraf Ghani ziliiambia Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), kwamba kurudi kwake hakukupangwa na serikali.
Zaidi ya watu 1000 waliandamana wakiongozwa na Atta Mohammad Noor , ambaye ni Gavana wa Kaskazini mwa mkoa wa Balkh kwa ajili ya kumpokea mpiganaji huyo wa zamani.
Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, mashahidi wanasema kuwa baadhi ya wafuasi wa Dostum walikuwa na mabango yaliyosema ‘karibu nyumbani kiongozi wetu,’.
Leave a comment