Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Makamu wa rais Afghanistan azuiwa kurudi nchini
Kimataifa

Makamu wa rais Afghanistan azuiwa kurudi nchini

Jenerali Abdul Rashid Dostum
Spread the love

MAKAMU wa rais wa Afghanistan, Jenerali, Abdul Dostum amezuiwa kuingia nchini mwake akitokea nchini Uturuki, anaandika Mwaandishi wetu.

Ndege ya kiongozi huyo iliyojaribu kutua nchini humo ikitokea Uturuki imezuiwa.

Dostum alijaribu kurudi nchini humo baada ya kusafiri kuelekea Uturuki mnamo mwezi Mei huku kukiwa na madai kwamba aliwaagiza watu wake kumteka, kumpiga na hata kumbaka mpinzani wake wa kisiasa.

Hata hivyo, amekana kufanya makosa yoyote na kuwa alielekea nchini humo kwa ukaguzi wa afya yake.Haijulikani ni nani aliyekataza kutua kwa ndege hiyo lakini taarifa za karibu na rais Ashraf Ghani ziliiambia Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), kwamba kurudi kwake hakukupangwa na serikali.

Zaidi ya watu 1000 waliandamana wakiongozwa na Atta Mohammad Noor , ambaye ni Gavana wa Kaskazini mwa mkoa wa Balkh kwa ajili ya kumpokea mpiganaji huyo wa zamani.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters, mashahidi wanasema kuwa baadhi ya wafuasi wa Dostum walikuwa na mabango yaliyosema ‘karibu nyumbani kiongozi wetu,’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!