Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Makamishna wa IEBC waliopinga matokeo watoa sababu nne
Kimataifa

Makamishna wa IEBC waliopinga matokeo watoa sababu nne

Spread the love

 

MAKAMISHNA wanne wa Tume Huru ya Mipaka na Uchaguzi ya Kenya (IEBC), wakiongozwa na Makamu Mwenyekiti, Juliana Cherera, wametaja sababu za kutokukubaliana na matokeo yaliyomtangaza William Ruto kuwa mshindi wa uchaguzi mkuu wa 2022. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kenya … (endelea).

Wakizungumza katika hoteli ya Serena wanne hao wamedai mwenyekiti, Wafula Chebukati, alipingana nao na kusisitiza kutangaza matokeo licha ya wasiwasi wao.

Pia wamedai kuwa hesabu za mwisho ya matokeo ya uchaguzi wa urais haikuletwa mbele ya tume ili kushughulikiwa.

Wakiorodhesha sababu nne za uamuzi wao wa kukataa matokeo yaliyotangazwa, makamishna hao wamesema kuwa ujumlishaji wa matokeo haukuwa sahihi kimahesabu na kwamba matokeo hayo hayajumuishi jumla ya waliojiandikisha kupiga kura, kura zilizopigwa au zilizokataliwa.

Chebukati alimtangaza Ruto jana kuwa mshindi wa uchaguzi mkuu kwa kura 7,176,141 sawa na asilimia 50.49% mbele ya mshindani wake Raila Odinga wa Muungano wa Azimio la Umoja aliyepata kura 6,942,930.

Ruto pia alitangazwa kushinda katika kaunti 39 kwa asilimia zaidi ya 25 ya kura halali ikiwa ni zaidi yatakwa la kikatiba linalomtaka mshindi wa uarais kushinda angalau katika kaunti 25 kwa kupata angalau asilimia 25 ya kura halali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!