Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Makalla apiga marufuku biashara kwenye barabara ya mwendokasi
Habari Mchanganyiko

Makalla apiga marufuku biashara kwenye barabara ya mwendokasi

Spread the love

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla leo tarehe 28 Januari 2023 ameongoza zoezi la usafi wilayani ya Temeke katika eneo la Mbagala na kupiga marufuku kufanya biashara kwenye  ujenzi wa barabara ya mwendokasi na maeneo yaliyokatazwa. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Makalla ametumia zoezi hilo kuwakumbusha wananchi na viongozi kuanzia ngazi ya mtaa hadi wilaya kuhakikisha wanasimamia usafi kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi.

Aidha RC Makalla amewaelekeza Wakurugenzi kusimamia wakandarasi kuondosha taka kwa wakati na wale watakaoonyesha kulegalega wasipatiwe mkataba.

Pia amewapongeza wananchi kufanya usafi jambo lililopelekea Jiji la Dar es salaam kushika nafasi ya sita kwa usafi Barani Afrika na kuondosha magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindipindu.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Machinga Mkoa wa Dar es salaam, zaidi ya Sh bilioni 3.2 zimetolewa kama  mkopo kwa wafanyabiashara wanaofanya biashara kwenye maeneo rasmi na kutoa wito kwa wafanyabiashara wengine kuacha kufanya biashara holela.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

error: Content is protected !!