Tuesday , 23 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Makaburi Pwani, Moro kuhamishwa kupisha Standard Gauge
Habari Mchanganyiko

Makaburi Pwani, Moro kuhamishwa kupisha Standard Gauge

Spread the love

SHIRIKA la Reli nchini (TRC) linatarajia kuhamisha makaburi kwenye mikoa ya Pwani na Morogoro ili kupisha ujenzi wa reli ya kisasa ‘Standar Gauge. Anaripoti Mwandishi Wetu …. (endelea).

Tangazo la uhamisho wa makaburi hayo limetolewa leo tarehe 24 Oktoba 2018 na Mkurugenzi Mkuu wa  Shirika la Reli nchini (TRC). Ambapo limetaja kuwa, makaburi hayo  yako ndani ya Halmashauri za Wilaya ya Kisarawe, Kibaha na Morogoro.

Kwa mujibu wa TRC, uhamisho huo utaanza kutekelezwa siku saba baada ya tangazo lake kutolewa.

“Katika halmashauri ya wilaya ya Kisarawe zoezi litafanyika kwenye kitongoji cha Kisarawe eneo la Mwambisi,  kwa upande wa Kibaha Vijijini litafanyika vijiji vya Soga, Magindu, Ngeta, Kikongo, Minazi Mikinda. Halmashauri ya wilaya ya Morogo uhamisho utafanyika vijiji vya Mgude, Mikese, na Mtego wa Simba.

Wakati Masnispaa ya Morogoro uhamisho utafanyika mtaa wa Seminari, Tungi, Kambi Tano na Tushikamane,” imeeleza TRC.

TRC imewataka wasimamizi wote kufika katika ofisi za maafisa watendaji wa vijiji na mitaa wa maeneo husika wakiwa na nyaraka zinazo watambulisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari Mchanganyiko

DC ampongeza Dk. Rose Rwakatare kwa kusaidia waathirika wa mafuriko Mlimba

Spread the loveMWENYEKITI wa Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk.  Rose Rwakatare...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!