Monday , 11 December 2023
Home Habari Mchanganyiko Makabila mchanganyiko kikwazo cha usafi Dar – Meya Moshi
Habari Mchanganyiko

Makabila mchanganyiko kikwazo cha usafi Dar – Meya Moshi

Moja ya sehemu chafu wa jiji la Dar es Salaam
Spread the love

MEYA wa Halmashauri ya Mji Moshi, Raymond Mboya amesema, mchanganyiko wa makabila katika Jiji la Dar es Salaam ni miongoni mwa vikwazo katika kutatua kero ya usafi. Anaripoti Hamis Mguta … (endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online ofisini kwake Moshi, Mboya ambaye ni Diwani wa Kata ya Longuo amesema, mji huo umefanikiwa kuwa msafi kutokana na elimu waliyopatiwa wananchi.

Na kwamba, uelewa walionao wakazi wa mji huo ni mkubwa ukilinganisha na wakazi wa Dar es Salaam kutokana na jiji hilo (Dar es Salaam) kuwa na mchanganyiko wa makabila huku kila moja lina utamaduni wake.

Mboya amesema, kutokana na mchanganyiko huo, umesababisha uongozi wa jiji hilo huo kupata shida katika kuhakikisha unakuwa safi.

“Dar es Salaam unaweza kupanga nyumba na ukawa mstaarabu na ukawa na elimu ya usafi wa mazingira, lakini utashangaa mwenzako anaweza akamwaga maji machafu mbele ya nyumba yake akaona ni kitu cha kawaida hivyo inachukua muda mrefu kumbadilisha mtu,”amesema.

Hata hivyo amesema kuwa, Halmashauri ya Mji wa Moshi wamejiwekea utaratibu maalum, ambao unamfanya mwananchi kutambua na kupokea elimu wanayopewa juu ya mazingira na miundombinu na kuwa, wameweka faini hata kwa anayetema mate.

“Moshi huwezi kumkuta mama ametoka jikoni na maganda ya vitunguu akamwaga mbele ya nyumba yake, hiyo kitu Moshi hakuna kwasababu watu wana uelewa wa kutosha kuhusu mazingira, nawapongeza watu wa Moshi. Moshi imekuwa ikiongoza kwa miaka mingi,” amesema.

Kuhusu mradi wa Soko Kubwa na Stendi katika mji huo Mboya amesema kuwa, wapo katika hatua nzuri za ujenzi huo ambapo hapo nyuma ilichukua muda kutokana na waziri aliyekuwa wa TAMISEMI, George Simbachawene kukwamisha miradi, hivyo baada ya kuwekwa Selemani Jafo ujenzi huo umeenda vizuri.

“Kwa sisi tulikuwa tunaona Simbachawene alikuwa anakwamisha maendeleo, lakini tunamshukuru Rais John Magufuli kwa kumuweka Jafo ili aendane na spidi yake na ametupa kibali tumeanza ujenzi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NBC yatoa msaada wa mil. 20 kwa waathirika mafuriko Hanang

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) sambamba na wafanyakazi wa...

Habari Mchanganyiko

Polisi wadaka mirungi kwenye basi la Extra Luxury

Spread the loveJeshi la polisi mkoani Kilimanjaro limekamata shehena ya dawa za...

Habari Mchanganyiko

Oryx yaungana na jamii kuwafariji waathirika maporomoko Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas Tanzania imeungana na Watanzania kutoa pole...

Habari Mchanganyiko

Amsons Group watoa milioni 100 waathirika maafa Hanang

Spread the loveKAMPUNI ya Amsons Group kupitia kampuni zake za Camel Oil...

error: Content is protected !!