HAYAWI hayawi sasa yamekuwa, Francis Ciza maarufu Majizo na Elizabeth Michael ‘Lulu’ wamefunga ndoa. Anaripoti Matrida Peter, Dar es Salaam..(endelea)
Majizo ambaye ni Mmiliki wa kituo cha radio na TV ya E-FM na TV-E amefunga pingu za maisha na Lulu, msanii wa maigizo nchini Tanzania, leo Jumanne tarehe 16 Februari 2021, katika Kanisa Katoliki la Mt. Maximilian Maria Kolbe Mwenge, jijini Dar es Salaa.
Wawili hao wamefunga pingu za maisha, baada ya kuwa kwenye mahusiano ya uchumba kwa zaidi ya miaka mitano.
Leave a comment