Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Majeshi ya nchi 7 kuonyesha umahiri Tanga
Kimataifa

Majeshi ya nchi 7 kuonyesha umahiri Tanga

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi
Spread the love

MAJESHI ya nchi saba za Jumuiya ya Maendeleo  ya  Afrika (SADC), yameanza mazoezi ya kijeshi yenye lengo la kujiandaa na tishio la mashambulizi ya kigaidi na uharamia yanayoitikisa dunia, anaandika Mwandishi wetu.

Akizungumza katika uzinduzi wa mazoezi hayo yanayozishirikisha nchi saba zilizopo kwenye jumuiya hiyo, Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, Dk Hussein Mwinyi, wanajeshi wa nchi hizo watabadilishana uzoefu wa namna ya kukabiliana na vitendo vya kigaidi na uharamia.

Dk Mwinyi ameeleza kuwa mazoezi hayo  yatawawezesha askari kupanua uzoefu katika masuala ya ulinzi na  kuimarisha  Umoja wa Maendeleo wa Nchi za Kusini (SADC).

“Tuna lengo la kujiweka tayari kwa misaada ya kijeshi katika kupambana na ugaidi na uharamia, baada ya hapo watapata uzoezfu mkubwa katika kukabiliana na vitendo hivyo vya kiharamia” amesema.

Ameeleza faida zitakazopatikana kutokana na mazoezi hayo  kufanyika Tanga na nchini kwa ujumla  ni pamoja na wananchi kupata tiba  kipindi chote cha mwezi mzima pamoja na ujenzi wa miundombinu.

Kwa upande wake,  Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Venance  Mabeyo  amesema zaidi  ya askari 600  kutoka nchi za Botswana, Lesotho, Zimbabwe, Afrika Kusini, Zambia, Malawi na Tanzania  watashiriki katika mazoezi hayo yatakayodumu kwa mwezi mzima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!