Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari Majaliwa: Madaktari endeleeni kumhudumia Mama yake Magufuli
Habari

Majaliwa: Madaktari endeleeni kumhudumia Mama yake Magufuli

Spread the love

 

WAZIRI Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema, madaktari wanaomhudumia Suzana, mama mzazi wa aliyekuwa Rais wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, wataendelea na jukumu hilo hadi mwisho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato…(endelea)

Majaliwa amesema, mama mzazi wa Hayati Magufuli, amekuwa mgonjwa kwa zaidi ya miaka miwili na Rais mpya wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, ametoa maagizo aendelee kuhudumiwa.

“Mama mzazi wa mpendwa wetu Dk. John Pombe Magufuli, yuko kitandani kwa zaidi ya miaka na maagizo yako mheshimiwa Rais, tunawataka madaktari kuendelea kumhudumia hadi atakaporudi kwenye uimara wa afya yake,” amesema Majaliwa

Dk. Magufuli alifariki dunia Jumatano ya tarehe 17 Machi 2021, katika Hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na unazikwa leo Ijumaa 26 Machi 2021, nyumbani kwao Chato mkoani Geita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!