Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Majaliwa ataka riba ya mikopo ipungue
Habari MchanganyikoTangulizi

Majaliwa ataka riba ya mikopo ipungue

Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Tanzania
Spread the love

SERIKALI imeitaka mifuko ya kijamii ambayo inatoa mikopo kwa jamii kufanya marekebisho upya ili kuona uwezekano kupunguza kiwango cha riba, anaandika Dany Tibason.

Kauli hiyo ilitolewa na Waziri Mkuu Kassimu Majaliwa, alipokuwa akizindua Baraza la Taifa la Uwezeshaji Kiuchumi, lililozinduliwa katika viwanja vya mashujaa Dodoma.

Majariwa amesema ili kutekeleza sera ya kumkwamua mwananchi katika hali ya umasikini ikiwa ni kupitia katika mifuko ya kijamii ni vyema sasa mifuko hiyo inafanya mapitio upya kwa lengo la kuangalia ni jinsi gani ya kuweza kupunguza riba.

Amesema kwamba jamii imekuwa haipati ujasiri wa kukopa mikopo kutoka kwenye mifuko ya kijamii kutokana na kuogopa riba kubwa ambayo inatolewa.

Katika hatua nyingine amewataka mawaziri pamoja na wakuu wa mifuko hiyo kuhakikisha anatoa elimu kwa jamii kwa lengo ya kuwapatia mikopo ambayo itawasaidia kuepukana na umasikini.

“Kwa sasa tumezindua baraza hili na ni mara ya kwanza kuzinduliwa rasmi tangu ianzishwe, hivyo basi mifuko hiyo inatakiwa kufanya kazi kwa uwazi kwa malengo ya kusaidia jamii na si vinginevyo.

“Ili kuweza kulifanya taifa kufikia sera ya Tanzania ya viwanda ni lazima kufanya linalowezekana kuhakikisha mwananchi wa kipato cha chini anawezeshwa na si kwa kumwekea riba kubwa katika mkopo au kumwekea masharti magumu,” amesema Majaliwa.

Pamoja na kuwepo mifuko hiyo pia amelitaka baraza la uwekezaji wananchi kiuchumi kufanya tathimini ya kuweza kuiunganisha mifuko hiyo kwa pamoja.

“Nalitaka baraza hili ifikapo Mei 28 mwaka huu nipewe majibu ya nini matokeo ya tathimini ambayo imefanyika kwa ajili ya kuunganisha mifuko ili kuachana na utitiri wa mifuko ambayo ipo kwa sasa,” amesema Waziri Mkuu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Baraza la Uwezeshaji Wananchi Taifa la Kiuchumi, Dk. John Jingu amesema jitihada sera ya serikali kuwa ya viwanda haziwezi kufanikiwa endapo hapatakuwa na ushirikiano kati ya serikali na wafanyabiashara.

Amesema kuwa moja ya vikwazo vya kutokufikia malengo kwa wananchi ni ukosefu wa mitaji, hivyo basi kwa kuwa mkuu wananchi kadhamilia kulifanya taifa kuwa na uchumi wa kati ni lazima wananchi wawezeshwe.

“Mifuko hii inatakiwa kujipanga na kuachana na tabia ya kufanya kazi kwa mazoea na kila mfuko uhakikisha unajenga kiwanda angalau kimoja katika maeneo yao ya kazi,” amesema Dk. Jingu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!